logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Magari mawili yateketea kufuatia ajali ya barabarani Machakos

Polisi na raia walikuwa kwenye eneo la tukio wakisaidia kuzima moto huo.

image
na

Habari17 February 2023 - 04:15

Muhtasari


•Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Machakos, Moss Ndhiwa alisema magari hayo ni trela ya futi 40 na gari la saloon.

Tukio la ajali ambapo magari mawili yaliteketea kwa moto kufuatia ajali ya barabarani katika mji wa Machakos mnamo Alhamisi, Februari 16, 2023.

Magari mawili yaliteketea Alhamisi usiku baada ya kushika moto kufuatia ajali iliyotokea katika mji wa Machakos.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Machakos, Moss Ndhiwa alisema magari hayo ni trela ya futi 40 na gari la saloon.

Ndhiwa alisema tukio hilo lilitokea kati ya vituo vya mafuta vya Shell na Rubis kwenye barabara ya Kyumbi-Machakos, mita chache kutoka Kituo cha Susu.

"Magari hayo mawili yaliungua kufuatia ajali ya barabarani. Tunajaribu kuuzima," Ndhiwa alisema kwenye simu Alhamisi usiku.

Alisema tukio hilo lilitokea dakika chache baada ya saa mbili jioni.

"Hatuwezi kutoa maelezo sasa, tuzime moto kwanza. Nitatoa maelezo baadaye," bosi huyo wa polisi aliongeza.

Polisi na raia walikuwa kwenye eneo la tukio wakisaidia kuzima moto huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved