logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera! Kenya yang'aa katika mbio za kupokezana vijiti za wanaume kwa wanawake

Emmanuel Wanyonyi, Mirriam Cherop, Kyumbe Munguti na Brenda Chebet waliipa timu ya Kenya ushindi

image
na Radio Jambo

Habari18 February 2023 - 06:54

Muhtasari


•Emmanuel Wanyonyi, Mirriam Cherop, Kyumbe Munguti na Brenda Chebet waliipa timu ya Kenya ushindi.

•Wanne hao waliipa Kenya dhahabu ya kwanza katika shindano hilo la kimataifa lililoanza  leo, Februari 18 asubuhi.

wametwaa ushindi katika mbio za kupokezana ushindi za wanaume kwa wanawake

Kenya imeibuka mabingwa wapya wa Dunia katika mbio za kupokezana vijiti za jinsia zote kwenye mashindano ya World Cross Country yanazoendelea.

Emmanuel Wanyonyi, Mirriam Cherop, Kyumbe Munguti na Brenda Chebet waliipa timu ya Kenya ushindi katika mbio hizo za wanaume na wanawake zilizofanyika jijini Bathurst, Australia siku ya Jumamosi asubuhi.

Mwanariadha wa mbio za mita 800 Emmanuel Wanyonyi ndiye alianza kwa upande wa Timu Kenya kabla ya kukabidhi kijiti kwa mwenzake Miriam Cherop huku Kenya ikienda nyuma ya wenyeji Australia mwishoni mwa mzunguko wa nne. Daniel Munguti kisha alipokea kijiti na kumpita Stewart Mcsweyn wa Australia kabla ya kumkabidhi  Brenda Chebet ambaye alihakikisha Kenya imepata ushindi.

Wanariadha wa Kenya walitumia muda wa dakika 23 na sekunde 21 mbele ya timu ya Ethiopia ambayo iliibuka ya pili kwa dakika 23, sekunde 23 huku wenyeji Australia wakifanikiwa kutwaa shaba kwa dakika 23 na sekunde 26. Afrika Kusini, Marekani na Uingereza kisha zilifuata kwa mpangilio wa mfululizo.

Wanne hao waliipa Kenya medali ya kwanza ya dhahabu katika shindano hilo la kimataifa lililoanza  leo, Februari 18 asubuhi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved