logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wafahamu wanasoka waliokufa chini ya mazingira yasiyo ya kawaida

Wachezaji 8 wa klabu ya Manchester United walifariki baada ya kuhusika katika ajali ya ndege mnamo Februari 6, 1958.

image
na Radio Jambo

Habari22 February 2023 - 12:24

Muhtasari


•Atsu ni miongoni mwa maelfu ya watu ambao wamepoteza uhai kufuatia tetemeko la ardhi ambalo lilikumba nchi ya Uturuki.

•Wachezaji 8 wa klabu ya Manchester United walifariki baada ya kuhusika katika ajali ya ndege mnamo Februari 6, 1958.

Hivi majuzi, habari za kuhuzunisha za kifo cha mchezaji wa Hatayspor, Christian Atsu, ambaye alipatikana amefariki chini ya vifusi vya nyumba katika mji wa Hatay zilivunja mioyo ya wengi kote duniani.

Atsu ni miongoni mwa maelfu ya watu ambao wamepoteza uhai kufuatia tetemeko la ardhi ambalo lilikumba nchi ya Uturuki mapema mwezi huu na kupelekea nyumba nyingi kuporomoka.

Kando na Atsu, kumekuwa na wachezaji wengine wengi ambao wamepoteza maisha yao ghafla  katika mazingira yasiyo ya kawaida.

Mnamo Aprili 27, 1993, ndege ya Jeshi la Wanahewa la Zambia iliyokuwa imebeba kikosi kizima cha timu ya taifa hilo (Chipolopolo) na wasaidizi wa kikosi  ilianguka katika Bahari ya Atlantiki muda mfupi baada ya kupaa kutoka Libreville, Gabon. Ajali hiyo ilisababisha vifo vya watu 30 wakiwemo wachezaji 18.

Wachezaji 8 wa klabu ya Manchester United walifariki baada ya kuhusika katika ajali ya ndege mnamo Februari 6, 1958.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved