logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mchezaji wa soka afariki akiwa uwanjani mechi ikiendelea

Sylla alihamia klabu yake mpya mwezi Septemba mwaka jana.

image
na Radio Jambo

Habari06 March 2023 - 08:45

Muhtasari


• Taarifa Zaidi kuhusu kifo cha mchezaji huyo hazijatolewa bado.

Moustapha Sylla, mcezaji wa Ivory Coast

Mchezaji wa soka nchini Ivory Coast katika ligi ya divisheni ya kwanza alifariki wikendi iliyopita wakati wa mechi.

Kulingana na taarifa za AFP, mchezaji hyo kwa jina Moustapha Sylla mweney umri wa miaka 21 alipatwa na matatizo ya kiafya wakati mechi ingali bado inaendelea na alikimbizwa hospitalini lakini akasemekana kufariki dunia.

"Beki wetu Moustapha Sylla alifariki jioni ya leo kufuatia kuugua uwanjani wakati wa mechi ya RCA vs Sol FC," ilisema taarifa ya klabu Racing d'Abidjan.

"Wakati wa kuhamishwa kwake hospitalini, Moustapha alifariki. Alifika klabuni Septemba mwaka jana na alikuwa na umri wa miaka 21 pekee," rais wa klabu Logossina Cisse alithibitisha kwa AFP.

Racing d'Abidjan walikuwa mabingwa wa kitaifa mwaka wa 2020 na kwa sasa wako nafasi ya saba kwenye michuano hiyo.

Taarifa Zaidi kuhusu kifo cha mchezaji huyo hazijatolewa bado.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved