logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 4 hufariki kila baada ya saa moja kutokana na makali ya HIV/AIDS, ripoti

Kaunti ya Homa Bay inaongoza kwa maambukizi ya ukimwi kwa asilimia 16.2

image
na Radio Jambo

Habari07 March 2023 - 10:51

Muhtasari


• Taarifa ya baraza hilo pia ilibainisha kuwa vifo 760,314 vimeepukika na Tiba ya Kuzuia Ukimwi (ART).

Mchoro wa ukimwi

Baraza la kitaifa la kudhibiti maambukizi ya Ukimwi limetoa takwimu za kushangaza kwamba angalau watu 4 hufariki kila baada ya saa moja kutokana na makali ya virusi vya Ukimwi.

Kulingana na ripoti ya siku ya Ukimwi Duniani ya 2022, Virusi vya ukimwi vilichangia asilimia 29 ya vifo vyote nchini. Kati ya kila watu wanne walioambukizwa KIV kwa saa mmoja alikuwa mtoto.

Taarifa ya baraza hilo pia ilibainisha kuwa vifo 760,314 vimeepukika na Tiba ya Kuzuia Ukimwi (ART).

Wakati huo huo, maambukizi ya watoto 164,072 yalizuiliwa kutokana na mpango wa Kuzuia Maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto.

Kaunti zilizo na maambukizi ya juu zaidi zilikuwa kama ifuatavyo: Kaunti ya Homa Bay ndiyo iliyokuwa na maambukizi ya KIV kwa asilimia 16.2, Kisumu (15.5%), Siaya (14.1%), Migori (10.4%), Busia (5.4%), Mombasa (5.4%). ), Kisii (4.7%), Samburu na Vihiga (4.6%), Nairobi (4.3%) na Uasin Gishu (4.0%).

Ripoti hiyo pia ilisema kuwa kuna mapuuza kwa baadhi ya watu kukosa kutumia dawa za kupunguza makali ya virusi hivyo huku ikisisitiza kwamba maombi kamwe hayawezi kutibu virusi vya ukimwi.

Mwezi jana, kulikuwa na mjadala mkali mitandaoni mchungaji mmoja maarufu nchini akidai kwamba aliwaponya mamia ya watu ambao walitafuta maombi katika mkusanyiko wake mkubwa na ambao walikuwa waathirika wa virusi vya ukimwi.

Wizara ya afya pia iliwataka walokole kutokosa kuhudhuria maombi lakini pia wasikose kutumia dawa za ARV kama wana virusi vya UKIMWI.

Mchoro wa ukimwi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved