logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wizara ya fedha yatangaza zabuni kudhibiti mende na panya

Lengo la programu ya AGPO ni kuimasha maisha ya vijana wanaweka na walemavu.

image
na

Habari07 March 2023 - 07:50

Muhtasari


• Ni sera ya serikali kwamba asilimia 30 ya zabuni zitolewe kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. 

Mende

Hazina ya Kitaifa imetangaza zabuni za huduma za ufukizaji na udhibiti wa wadudu wakiwemo panya, fursa ambayo imetengwa kwa ajili ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu pekee. 

Katika tangazo lililolipiwa, wizara ilisema hati za zabuni zinaweza kupakuliwa bila malipo kwenye tovuti yake. 

"Zabuni hii imetengewa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu pekee," lilisema tangazo hilo.

Hati za zabuni zilizokamilishwa zitapelekwa kwenye Jengo la Hazina mnamo au kabla ya tarehe 21 Machi 2023, saa tano mchana. 

"Zabuni zitafunguliwa mara moja mbele ya wazabuni au wawakilishi wao waliowachagua kuhudhuria ufunguzi katika Jengo la Hazina saa tano asubuhi saa za Kenya," wizara ilisema. 

Serikali imekuwa ikifanya juhudi za makusudi kushughulikia kwa dhati matatizo ya vijana kuanzia ukosefu wa ajira, umaskini na ujuzi usiotumika.  

Ni sera ya serikali kwamba asilimia 30 ya zabuni zitolewe kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. 

Sera hiyo inatekelezwa katika muktadha wa Mpango wa Upatikanaji wa Fursa za Ununuzi Serikalini (AGPO) ambao ulizinduliwa rasmi na Rais mstaafu Uhuru Kenyatta mnamo Oktoba 16, 2013. 

AGPO imeegemezwa kwenye Kifungu cha 227 cha Katiba kuhusu ununuzi wa bidhaa na huduma wa umma wenye usawa, wa uwazi na wa gharama nafuu.Pia inatokana na Kifungu cha 55 cha mwaka 2010 kuhusu hatua za uthibitisho na Sheria ya Ununuzi wa Umma na Uondoaji wa Mali, 2015.

Lengo la programu ya AGPO ni kuwezesha makampuni yanayomilikiwa na wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ili kuweza kushiriki katika fursa za Serikali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved