logo

NOW ON AIR

Listen in Live

IPOA yaanzisha uchunguzi wa mauaji ya wanaume 2 Murang'a

Makori aliongeza kuwa hatua zinazofaa zitachukuliwa baada ya uchunguzi kukamilika.

image
na Radio Jambo

Habari13 March 2023 - 12:28

Muhtasari


  • Katika taarifa kutoka kwa mwenyekiti Anne Makori siku ya Jumatatu, IPOA ilisema timu tayari imetumwa katika eneo hilo

Mamlaka Huru ya Uangalizi wa Polisi (IPOA) imeanzisha uchunguzi kuhusu mauaji ya wanaume wawili waliouawa kwa kupigwa risasi Jumapili Murang'a.

Katika taarifa kutoka kwa mwenyekiti Anne Makori siku ya Jumatatu, IPOA ilisema timu tayari imetumwa katika eneo hilo na tangu wakati huo imebaini kuwa maafisa wa polisi walikuwa sehemu ya tukio hilo.

Makori aliongeza kuwa hatua zinazofaa zitachukuliwa baada ya uchunguzi kukamilika.

Haya yanajiri huku kukiwa na maswali mengi kutoka kwa umma baada ya kifo cha wawili hao kuripotiwa kwa njia isiyo ya kawaida na Kurugenzi ya Upelelezi wa Jinai (DCI).

DCI, katika kisa hicho, iliripoti kuwa washukiwa hao walipigwa risasi baada ya "makabiliano makali ya risasi na maafisa wa polisi" katika eneo la Kigumo, kaunti ya Murang’a Jumapili asubuhi.

Ripoti hiyo ilizua hisia tofauti mitandaoni baada ya uvumi kuwa maafisa wa polisi walikuwa wamewakamata wawili hao hapo awali.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved