logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tunajiunga na chama kinachojali watu wake-Kidero baada ya kujiunga na UDA

Aidha, alisema kuwa hawatashiriki maandamano ya Azimio yanayoendelea

image
na Radio Jambo

Habari14 March 2023 - 11:05

Muhtasari


  • Viongozi hao walisema kuwa watafanya kazi na Serikali ya Kenya Kwanza kuhakikisha maendeleo katika mikoa ya Nyanza

Viongozi wa Nyanza wakiwemo waliokuwa magavana Evans Kidero (Nairobi), Okoth Obado (Migori) na Jack Ranguma (Kisumu), wamethibitisha kujiunga na chama kinachoongozwa na Rais William Ruto United Democratic Alliance (UDA) 

Viongozi hao walisema kuwa watafanya kazi na Serikali ya Kenya Kwanza kuhakikisha maendeleo katika mikoa ya Nyanza.

Akizungumza wakati na waandishi wa habari katika makao makuu ya Chama cha UDA mnamo Jumanne, Machi 14, Kidero alisema kuwa chama tawala kinawajali watu wa Kenya na kuongeza kuwa muungano wa Azimio ulizingatia jambo lisilofaa.

Aidha, alisema kuwa hawatashiriki maandamano ya Azimio yanayoendelea na kuongeza kuwa yanawatenga Waluo Nyanza kutoka maeneo mengine ya nchi.

Tumesikia kuhusu maandamano na yatasababisha watu kuteseka. Tunaingia kwenye chama kinachojali watu wake na sio chama tulichoacha chenye nia ya machafuko.

"Chama kina nia ya kujifanyia mambo yao wenyewe na sio watu waliowachagua. Kulikuwa na maandamano Migori na mama zetu hawakuweza kuuza Omena kwa sababu shughuli za kawaida zililemazwa," Kidero alilalamika.

Zaidi ya hayo, Kidero alibainisha kuwa licha ya jamii ya Waluo Nyanza kutompigia kura Rais na Naibu Rais, wameweka eneo hilo kipaumbele linapokuja suala la maendeleo.

“Katika muda wa miezi mitatu, yeye (Rais) amewahakikishia watu wa Nyanza kwamba lazima tuwe sehemu ya Kenya. Tumeona ahadi ya Rais ya kujenga barabara mbalimbali za Siaya, Kisumu, Homabay na Migori,” akaongeza.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved