logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Willy Paul amfichua Zuena wake

Msanii Willy Paul alimfichua Zuwena wake aliyedai kuwa angewatambulisha kwa mashabiki wake karibuni.

image
na Radio Jambo

Habari14 March 2023 - 05:11

Muhtasari


•Msanii Willy Paul alidai kuwa alimlipa Zuwena wake shilingi milioni 2 ili kucheza kama vixen kwenye video yake.

Msanii Willy Paul almaarufu Pozee  alimfichua Zuwena wake aliyedai kuwa angewatambulisha kwa mashabiki wake karibuni.

Zuwena wake Willy Paul  haikuwapata mashabiki kwa mshtuko kwa sababu huyo Zuwena ni msanii wa Tanzania, Nandy.

Willy Paul alisema kwenye mtandao wa Instagram kuwa alibaki kapera kwa ajili ya Nandy na kuonekana kuwa wako kwenye harakati  kutengeneza kibao na na Nandy huu wakisema atapeana habari zaidi.

"Mshangao kwenu,ndiye huyu hapa, Nandy, nimekuwa kapera  kwa ajili ya huyu,habari zaidi inakuja,"

Msanii Willy Paul alidai kuwa alimlipa Zuena wake shilingi milioni 2 ili kucheza kama vixen kwenye video yake.

Willy Paul aliwakashifu wale waliomsuta wakisema kuwa alinakili wazo wa wimbo wake msanii wa Tanzania Diamond Platinumz aliyetoa kibao cha Zuwena mwezi mmoja uliopita.Pozze alisema aliwakejeli kwa kusema shilingi milioni 2 alizomlipa zilikuwa za Kenya na si Tanzania.

"Baada ya kusikiliza kisa cha Zuena ilibidi nimweke Zuena huyo huyo kwenye wimbo, sioni shida yoyote ,elewa kwa upole ,si jambo zito"alisema mtanadaoni.

Willy Paul pia alidai pia kuwa Zuwena aliyemtumia kama vixen ni mrembo mara hamsini zaidi ya ule wa wimbo asili wa Zuwena wake Diamond.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved