logo

NOW ON AIR

Listen in Live

RIP: Afrika Kusini yapoteza msanii mwingine wa tatu ndani ya wiki tano

Bosman, msanii wa Jazz alifariki akiwa na umri wa miaka 50.

image
na Radio Jambo

Habari15 March 2023 - 07:21

Muhtasari


• Mwanamuziki huyo hivi majuzi aliteuliwa katika bodi ya Samro (shirikisho la hakimiliki za wasanii wa Afrika Kusini) kama mkurugenzi asiye mtendaji.

• Hata hivyo, Samro hawakuweka wazi kiini cha kifo cha malikia huyo wa Jazz.

Gloria Bosman, msanii wa Jazz aliyefariki.

Kwa mara nyingine tena, taifa la Afrika Kusini limetupwa kwelie kipindi cha maombolezo. Hii ni baada ya taarifa za kifo cha msanii mwingine, Gloria Bosman, aliyekuwa msanii wa Jazz.

Gloria Bosman, alifariki akiwa na umri wa miaka 50 na taarifa zake kulingana na jarida la Soweto, zilifichuliwa na shirikisho la hakimiliki za kkazi za Sanaa za wasanii wa taifa hilo lenye raia wenye rangi ya ngozi ainati.

Mwanamuziki huyo hivi majuzi aliteuliwa katika bodi ya Samro (shirikisho la hakimiliki za wasanii wa Afrika Kusini) kama mkurugenzi asiye mtendaji.

Bosman alizaliwa Mofolo katikati mwa Johannesburg na kukulia Pimville, Soweto. Anajivunia Tuzo mbili za Muziki za Afrika Kusini (Samas) na uteuzi zaidi ya 11, pamoja na uteuzi wa Kora mara mbili, Soweto Live waliripoti.

Albamu ya kwanza ya Bosman, Tranquility, ambayo ilitolewa katika miaka ya 1990, ilimletea tuzo ya heshima ya Mgeni Bora na kupokea uteuzi wa Albamu Bora ya Kisasa ya Jazz na Msanii Bora wa Kike katika Samas za 2001.

 

Kifo cha msanii huyo maarufu wa Jazz kinakuja siku chache tu baada ya kifo cha msanii wa Amapiano, Costa Titch kuzuka.

Titch, bingwa wa Amapiano alifariki baada ya kudondoka jukwaani alikokuwa akitumbuiza, kulingana na mikanda ya video ambayo imekuwa ikisambazwa na kuenezwa mitandaoni.

Vifo vya wawili hawa vinakuja chini ya wiki tano tu baada ya kifo cha ghafla mno cha msanii AKA ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana ambao walimvizia kwenye mmgahawa mmoja nchini humo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved