logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Marekani yatishia kuipiga marufuku TikTok iwapo haitauzwa – ripoti

Marekani inasema TikTok lazima iuzwe la sivyo ikabiliwe na uwezekano wa kupigwa marufuku nchini humo

image
na Radio Jambo

Habari16 March 2023 - 08:02

Muhtasari


•Programu hiyo inashutumiwa kwa kusababisha hatari ya usalam wa taifa kwa kukusanya data kutoka data za mamilioni ya watumiaji.

Serikali ya Marekani inasema TikTok lazima iuzwe la sivyo ikabiliwe na uwezekano wa kupigwa marufuku nchini humo, kwa mujibu wa ripoti.

Programu (app) hiyo ya kushirikisha video, inayomilikiwa na kampuni ya Kichina Byte Dance, inashutumiwa kwa kusababisha hatari ya usalam wa taifa kwa kukusanya data kutoka data za mamilioni ya watumiaji.

Ombi la kubadili umiliki, kwa mara ya kwanza liliripotiwa katika jarida la Wall Street Journal (WSJ), lilithibitishwa kwa BBC na TikTok.

Kampuni hiyo inasema mauzo ya kulazimishwa hayatabadili usambaaji wa data au upatikanaji wa programu ya TikTok.

Ikulu ya White House bado haijajibu ombi la BBC News la kutaka kauli yake.

Kwa miaka maafisa wa Marekani wamekuwa wakielezea hofu zai kwamba taarifa(data) kutoka kwa app hiyo maarufu zinaweza kuangukia mikononi mwa serikali ya Uchina.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved