logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila ana mamilioni ya wafuasi wanaomwabudu-Alinur asema huku akimshauri Rais haya

Pia waziri huyo wa zamani alidai kwamba hataki hendisheki na mkuu wa nchi.

image
na Radio Jambo

Habari16 March 2023 - 09:45

Muhtasari


  • Matamshi ya Alinur yanajiri saa chache baada ya seneta wa Nairobi Edwin Sifuna kusema kwamba Serikali ilikaidi wito wao wa mazungumzo.

Mwanasiasa na mfuasi sugu wa Azimio Alinur Mohamed amemtaka rais William Ruto nanaibu wake Rigathi Gachagua kumtafuta waziri mkuu wa zamani Mhe Raila Odinga wafanye mazungumzo naye kabla mambo hayajaharibika.

Kulingana naye waziri mkuu wa zamani Mhe Raila Odinga bado ana mamilioni ya wafuasi wanaomwamini licha ya kushindwa katika uchaguzi wa urais wa 2022.

"Rais William Ruto na Naibu wake Rigathi Gachagua wanapaswa kumtafuta Raila Odinga na kuzungumza kama waungwana. Kenya ni kubwa kuliko sisi sote. Hatuwezi kufikiria hali ambapo Kenya inakuwa Sudan mpya. Raila ana mamilioni ya wafuasi wanaomwabudu, hatuwezi kupuuza hilo". Alisema Mhe. Alinur Mohamed.

Kumbuka kuwa rais William Ruto yuko kwenye rekodi akidai kuwa hatakubali hendisheki na aliyekuwa waziri mkuu Mh Raila Odinga kama serikali iliyopita.

Pia waziri huyo wa zamani alidai kwamba hataki hendisheki na mkuu wa nchi.

Matamshi ya Alinur yanajiri saa chache baada ya seneta wa Nairobi Edwin Sifuna kusema kwamba Serikali ilikaidi wito wao wa mazungumzo.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved