logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Andrew Kibe afichua mastaa ambao 'wamemblock' kwenye Instagram

Andrew Kibe alidai kuwa anachokosoa kwa mastaa hao ni mienendo yao tu lakini hana ubaya.

image
na

Habari22 March 2023 - 06:43

Muhtasari


• Andrew Kibe amejipata katika ugomvi na vita vya mtandao kati yake na baadhi ya mastaa kwa kuwakashifu kwa kile anachodai ni mienendo mibovu.

Marua amjibu Kibe

Aliyekuwa mtangazaji wa redio , Andrew Kibe amewataja mastaa ambao wamempa 'block' kwenye Instagram.

Kibe alidai kuwa wale waliompiga block hawana ufahamu wa burudani na showbiz.

Baadhi yao alisema wamemzuia ni pamoja na Pulse Live, aliyekuwa mtangazaji wa radio Kamene Goro, Terence Creative na mke wake Milly.

Kibe alisema hahisi vizuri kwa sababu hakuwa na ubaya ila anajaribu kukosoa tabia zao tu.

Ingawa  ana ugomvi na Diana B, Kibe alisema kuwa Diana hajamblock. Hivi majuzi, Diana B alisema kuwa hana ubaya na Andrew Kibe na kwamba ni burudani tu anafanya.

Bahati na Diana walionekana kutokerwa na kashfa za Andew Kibe kwao kwenye mtandao.

Presenter Ali pia alitajwa kama mtu aliyempiga block Andrew katika mtandao wa Instagram. Kibe alisema kuwa walikosea hivyo basi wakubali kukashifiwa na wapate kujifunza kutokana na kashfa hiyo.

Kibe aliongezea kuwa Jalas hajampiga block kwa sababu yeye anaelewa burudani.

Alitaja NRG radio pia kuwa kama mojawapo ya stesheni na watu waliomblock. Kibe alieleza mshangao wake ni kwanini stesheni aliyoifanyia kazi wamembock kwenye Instagram hivyo akidai aliyesababisha hilo ni Mwalimu Rachel.

Andrew Kibe alieleza kuwa hana jambo zuri wala baya la kusema kuhusu mwalimu Rachel ila atachunguza ili ajue nini kilisababisha hatua hiyo.

Andrew Kibe kwa sasa amejipata katika ugomvi na vita vya mtandao kati yake na baadhi ya mastaa kwa kuwakashifu kwa kile anachodai ni mwenendo mbaya wa maisha.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved