logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Eric Omondi ataka maandamano yawe Jumatatu hadi Jumatatu

Eric Omondi alitaka maandamano kuundelea hadi serikali ipunguze gharama ya maisha.

image
na

Habari22 March 2023 - 06:54

Muhtasari


•Omondi alisema iwapo Azimio hawataweka maandamano kila siku, yeye atweka yake siku ya Jumatano na Ijumaa.

Msanii Eric Omondi amemwomba kinara wa Azimio Raila Odinga kuweka maandamano kila siku.

Eric amedai kuwa maandamano ya kila siku ili kukwamisha shughuli zote nchini. 

Omondi alimsuta naibu rais Rigathi Gachagua kwa kusema kuwa wawekezaji na wafanyibiashara walipoteza pesa nyingi kutokana na maandamano na ilhali yeye, rais William Ruto na mkuu wa mawaziri Musalia Mudavadi walijitengea shilingi milioni 802 kununua magari mapya.

"Ningependa kumwomba mheshimiwa Raila Odinga kufanya maandamano kila siku kuanzia Jumatatu hadi Jumatatu...Gachagua alisema kuwa serikali inapoteza ila walipewa shilingi 802 milioni kununua magari," alisema Omondi.

Omondi alisema maandamano yatafanya serikali pia kupoteze pesa kama hali ilivyo kwa wananchi wa kawaida. Aliongezea kuwa wako tayari kujiunga na maandamano hayo.

Eric alidai kuwa idadi kubwa ya Wakenya wanahangaika ilhali wachache ndio wanapata raha hivyo basi ni bora kila mtu awe sawa kwa kuhangaika.

Alisema haya huku akitoa mfano wa vijana aliowalipia faini ili waachiliwe kutoka korokoroni kwa kukosa shilingi mia tano.

Alipoulizwa kuhusu viongozi kufanya mazungumzo, msanii huyo mwenye miaka 41 alidai kuwa kuongea kutafanywa wakati serikali itashusha gharama ya maisha ili watu wasiumie zaidi.

Eric Omondi amekuwa akiandaa maandamano katika majengo ya bunge dhidi ya gharama ya juu ya maisha. Mara ya mwisho alishikwa na polisi na kuachiliwa kwa dhamana ya pesa taslimu 150,000.

Kinara wa muungano wa Azimio, Raila Odinga, ameitisha kufanyika kwa maandamano ya amani siku za Jumatatu na Alhamisi, kila wiki.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved