logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Refa afutwa kazi kwa kutumia video iliyorekodiwa na shabiki kufuta bao la timu pinzani

Mwamuzi alikubali pendekezo hilo na alifuta bao baada ya kukagua eneo la tukio.

image
na Radio Jambo

Habari23 March 2023 - 06:34

Muhtasari


• Awali mchezo huo ulisimama kwa takriban dakika 20 kutokana na pingamizi la viongozi wa El Suez waliomtaka mwamuzi kuangalia goli kwenye kioo cha simu ya mkononi.

• Mechi iliyoisha kwa ushindi wa mabao 3-1 kwa Montakhab El-Suez.

Mwamuzi akipitia bao kwenye kioo cha simu ya mkononi

Kamati ya waamuzi ya Shirikisho la Soka la Misri (EFA) iliamua Jumanne kumsimamisha kwa muda usiojulikana mwamuzi wa mchezo kati ya Montakhab El-Suez na El-Nasr katika mchezo wa ligi daraja la pili siku ya Ijumaa.

Inaarifiwa kwamba refa huyo alitumia video iliyorekodiwa katika simu ya shabiki mmoja na kuitumia kama kigezo cha kufuta bao la El-Nasr kwa madai kwamba lilikuwa bao la kuotea.

“Mwamuzi alighairi bao la El-Nasr baada ya kuangalia skrini ya simu ya rununu kuthibitisha mchezaji wa El-Nasr aligusa mpira kwa mkono wake kabla ya kufunga bao,” sehemu ya taarifa ya madai hayo ilisoma.

Picha zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ya Misri zikimuonyesha mwamuzi akiangalia goli kwenye skrini ya simu ya mkononi, jambo lililosababisha dhihaka za watazamaji.

Kulingana na afisa wa Montakhab El-Suez, tukio lilianza wakati mchezaji wa El-Nasr alipoifungia timu yake bao la kusawazisha huku matokeo yakiwa 2-1 kwa upande wa timu El Suez.

Awali mchezo huo ulisimama kwa takriban dakika 20 kutokana na pingamizi la viongozi wa El Suez waliomtaka mwamuzi kuangalia goli kwenye kioo cha simu ya mkononi.

Mwamuzi alikubali pendekezo hilo na alifuta bao baada ya kukagua eneo la tukio.

Uamuzi huo uliibua hasira za viongozi wa El-Nasr na mchezo ukasimama kwa dakika nyingine 15 kabla ya kuendelea na mechi iliyoisha kwa ushindi wa mabao 3-1 kwa Montakhab El-Suez.

Mapema wiki hii, kamati ya mashindano ya EFA iliridhia matokeo ya mchezo huo na kuwatoza faini maafisa kadhaa wa vilabu vyote viwili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved