logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanafunzi 124 wa shule ya upili ya Mukumu Girls waugua kuhara

Maafisa walisema kuwa ulaji wa chakula kilichoathirika inaweza kuwa sababu ya wanafunzi hao kuhara.

image
na

Habari28 March 2023 - 15:07

Muhtasari


•Vipimo vya awali vilivyofanywa na maafisa wa afya ya umma vilitupilia mbali ugonjwa wa Kipindupindu.

•Maafisa hao walisema kuwa ulaji wa chakula kilichoathirika inaweza kuwa sababu ya wanafunzi hao kuhara.

Takriban wanafunzi 124 wa Shule ya wasichana ya Sacred Hearts Mukumu katika kaunti ya Kakamega wamelazwa katika hospitali ya Kakamega County General.

Ingawa haijabainika mara moja kile ambacho kinawaathiri wanafunzi hao, vipimo vya awali vilivyofanywa na maafisa wa afya ya umma vilitupilia mbali ugonjwa wa Kipindupindu.

Maafisa hao walisema kuwa ulaji wa chakula kilichoathirika inaweza kuwa sababu ya wanafunzi hao kuhara.

Afisa mkuu wa afya katika kaunti ya Kakamega, David Alila alisema kuwa wanafunzi zaidi wanaendelea kupokelewa katika hospitali hiyo.

"Bado hatujajua sababu halisi ya kuhara ni nini. Bado tunaendelea na vipimo,” alisema.

Alisema hospitali hiyo itatoa ripoti ya kina baada ya kukamilisha vipimo.

Juhudi za kupata maoni kutoka kwa mkuu wa shule Fridah Amwayi hazikufua dafu kwani hakujibu simu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved