logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wataalamu wa ndani ndio wanawasaidia wanariadha wa Kenya kudanganya – Shirika la AIU

Nalyanya na Lempus, walidaiwa kutoa karatasi ghushi kuunga mkono madai yao ya kudungwa sindano ya misuli katika hospitali moja.

image
na Radio Jambo

Habari05 April 2023 - 07:37

Muhtasari


•Kitengo cha Uadilifu wa Riadha kilifikia hitimisho hilo baada ya wanariadha wawili kutumia hadithi sawa kuelezea makosa ya matibabu.

Kenya ni nyumbani kwa wanariadha wanaobobea dunia

Shirika linalosimamia mpango wa kupambana na matumizi ya dawa za kusisimua misuli kwa wanariadha wa kimataifa limesema kuwa wanariadha wa Kenya wanasaidiwa na wataalam wa matibabu wa nchini humo ili kuficha makosa ya matumizi ya dawa hizo.

Kitengo cha Uadilifu wa Riadha kilifikia hitimisho hilo baada ya wanariadha wawili kutumia hadithi sawa kuelezea makosa ya matibabu.

Wakimbiaji hao, Eglay Nafuna Nalyanya na Betty Lempus, walidaiwa kutoa karatasi ghushi kuunga mkono madai yao ya kudungwa sindano ya misuli katika hospitali moja.

Riadha Kenya ilisema wiki jana kwamba ilikuwa imeahidiwa $5m (£4m) kwa mwaka kukabiliana na matumizi ya dawa za kusisimua misuli.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved