logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ningewaajiri Diana Marua na Bahati wakuwe wakinioshea gari langu-Kibe azungumzia utajiri wa Hakimi

Kibe alisema kuwa jambo moja ambalo angeweza kufanya ni kuwaajiri Bahati na Diana waoshe gari lake.

image
na Radio Jambo

Habari17 April 2023 - 10:58

Muhtasari


  • Alisema kama angekuwa anapokea mshahara mkubwa kama nyota huyo wa PSG basi angeweza kuwa na kiburi na mjeuri zaidi.
Marua amjibu Kibe

Mmoja wa watu mashuhuri wa kenya na mtayarishaji maudhui anayeishi Marekani, Andrew Kibe, amewasuta Bahati na Diana Marua kwa mara nyingine.

Kibe huwa anapinga uhusiano wao, na katika podikasti yake, kila mara hutumia bahati na Diana kama mifano.

Wakati akizungumzia suala la Hakimi, Kibe aliamua kuwahusisha Bahati na Diana kwenye hadithi hiyo, kwa kuwatumia kama mfano.

Alisema kama angekuwa anapokea mshahara mkubwa kama nyota huyo wa PSG basi angeweza kuwa na kiburi na mjeuri zaidi.

Kibe alisema kuwa jambo moja ambalo angeweza kufanya ni kuwaajiri Bahati na Diana waoshe gari lake.

Kulingana na yeye, hii ingewezekana kupitia wakala wao. Angeweza kuwalipa hadi ksh.240,000 kwa kila kipindi cha kuosha, ili kuwaonyesha kwamba yeye ni tajiri.

Alisema kwamba wanandoa wanapaswa kumshukuru Mungu kwa kuwa hapokei mshahara mkubwa kila wiki kama Hakimi.

Hata hivyo ikiwa hilo litatokea katika siku zijazo, basi hatasita kuwaajiri wawili hao kuosha gari lake.

Zaidi ya hayo hakuna Mkenya ambaye angeweza kumwambia chochote, kwa sababu angeweza kukosa heshima ikilinganishwa na sasa.

Ijumaa kulikuwa na taarifa ambazo hazijadhibitishwa kwamba mchezaji wa kimataifa wa Morocco na timu ya PSG, Achraf Hakimi alikuwa amemrithisha mama yake mali yake yote.

Hili lilibainika baada ya mke wake raia wa Uhispania kupeleka kesi ya talaka mahakamani akidai Zaidi ya asilimia 50 ya mali ya beki huyo, lakini akapigwa na butwaa baada ya mahakama kubaini kwamba mchezaji huyo hakuwa na mali yoyote chini ya jina lake, bali mali yote yaliandikishwa kwa jina la mamake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved