logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zuchu amkosha Stevo Simple Boy baada ya kujirekodi akiiga sauti yake

Zuchu alikuwa akiiga sauti ya Stevo akiwapuuzilia mbali wapenzi wazamani.

image
na Radio Jambo

Habari18 April 2023 - 07:55

Muhtasari


• Rapa huyo alizidi kumshukuru Zuchu kwa kumuiga.

• Katika kujibu kwa haraka, Stivo Simple Boy aliingia kwenye akaunti yake ya Instagram na kushiriki upya video ya Zuchu akimuiga.

Stevo afurahia Zuchu kumuiga

Msanii Stevo Simple Boy ni mwenye furaha ya mbingu ya saba baada ya malkia wa Bongo Fleva Zuchu kufanya skit ya TikTok akiiga sauti ya msanii huyo.

Zuchu alipakia klipu hiyo akiiga sauti ya Stevo Simole Boy ambayo alikuwa akizungumzia kuhusu mpenzi wa zamani, akilenga mkuki wake kwenye kambi ya aliyekuwa mpenzi wake Pritty Vishy kuwa hafai kumkaribia kabisa, na msanii huyo wa Kenya alipakia klipu hiyo akionesha furaha yake tele.

"Ma-ex wakae kando sahi nko na barafu wangu wa moyo. [Ananipea] mahaba, kunikanda ehh kuniandalia mamkuli," Zuchu alisema huku akimuiga Stivo Simple Boy.

Katika kujibu kwa haraka, Stivo Simple Boy aliingia kwenye akaunti yake ya Instagram na kushiriki upya video ya Zuchu akimuiga.

Rapa huyo alizidi kumshukuru Zuchu kwa kumuiga.

“Haya hata @officialzuchu ashasema ma ex wakae kando Habari iwafikie jamani wengine tuna barafu wetu wa moyo 😂😂😂❤️,” Stivo aliandika.

Hata hivyo, baadhi ya mashabiki wa Stevo walimtaka kutumia fursa hiyo na kumuomba Zuchu mkono katika kushirikiana pamoja kufanya collabo.

“Stevo sasa usilalishe, tumia fursa hii kuomba collabo kwa mpenzi wa Diamond. Fom imejipa,” mmoja alimshauri.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved