logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii wa kibao cha Firirinda Dickson alazwa hospitalini

'Firirinda' ya Munyonyi ilivuma mitandaoni kwenye TikTok mwaka wa 2021,

image
na Radio Jambo

Yanayojiri20 April 2023 - 11:20

Muhtasari


  • Mwanamuziki huyo ambaye alianza kazi yake ya muziki mwaka wa 1971 na hata kutumbuiza katika harusi ya aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta mnamo 1989, ameanza matibabu

Nyota wa nyimbo za  Mugiithi Dick Njoroge Munyonyi,  kwa wimbo wake maarufu wa 'Firirinda,' hivi majuzi alifichua kwamba alipatikana na saratani ya kibofu.

Mwanamuziki huyo ambaye alianza kazi yake ya muziki mwaka wa 1971 na hata kutumbuiza katika harusi ya aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta mnamo 1989, ameanza matibabu ana matumaini ya kupona hivi karibuni.

Kwa bahati mbaya, masuala ya afya ya Munyonyi hayajaishia hapo. Kwa sasa amelazwa hospitalini, akipambana na kifua kikuu, kulingana na vyanzo. Haijulikani ikiwa utambuzi wake wa kifua kikuu unahusiana na utambuzi wake wa saratani.

Habari za kulazwa kwa Munyonyi zimeibua sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki na wanamuziki wenzake katika tasnia hiyo. Wengi wanatuma salamu zao za heri na kutoa msaada wao, huku wengine wakitaka kuchangisha fedha za matibabu ili kusaidia kugharamia matibabu ya msanii huyo.

'Firirinda' ya Munyonyi ilivuma mitandaoni kwenye TikTok mwaka wa 2021, zaidi ya miongo mitatu baada ya kuachiliwa kwa mara ya kwanza, na hivyo kumvutia msanii huyo kujulikana. Mchanganyiko wake wa kipekee wa muziki wa Kikuyu na Mugithi umemfanya kupendwa sana katika tasnia hiyo, na matatizo yake ya kiafya yamewaacha wengi wasiwasi kuhusu ustawi wake.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved