logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wakili Miguna amsuta DCI kwa uamuzi wake kuhusu kifo cha Jeff

Hii imezua taharuki miongoni mwa Wakenya.

image
na Radio Jambo

Habari22 April 2023 - 21:56

Muhtasari


  • Ripoti za awali zilizotolewa na DCI zilionyesha kuwa Jeff aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa nje ya nyumba.

Wakili Miguna Miguna amevunja ukimya wake baada ya maafisa wa DCI kusema kuwa Jeff Mwathi alifariki kutokana na kujitoa uhai.

Ripoti za awali zilizotolewa na DCI zilionyesha kuwa Jeff aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa nje ya nyumba.

Aidha, taarifa hizo pia zilionyesha kuwa haiwezekani kwa mtu yeyote wa umri kupita kwenye grili za madirisha nyumbani kwa DJ Faxto.

Ripoti ya hivi punde iliyotolewa na DCI ilifichua kuwa Jeff alijitoa uhai kwa kuruka kutoka kwa nyumba ya Faxto kupitia dirishani.

Hii imezua taharuki miongoni mwa Wakenya.

Wakili Miguna amekashifu DCI kuhusu uamuzi wake kuhusu kifo cha Jeff Mwathi. Kulingana na Miguna, Jeff Mwathi aliuawa kabla ya kutupwa nje ya nyumba.

"Kuhusu uchunguzi wa MAUAJI ya Geoffrey Mwathi, maoni yangu ni kwamba @DCI_Kenya wachunguzi wameonyesha kutokuwa na uwezo na/au maelewano ya kimaadili. Mwathi aliuawa na kutupwa nje ya jengo. Hadithi nyingine yoyote ni hogwash."

Katika taarifa iliyotolewa na DCI, ilisema kuwa DJ Faxto hakuhusishwa na kifo cha Jeff kwa sababu hawakuwa na ushahidi.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved