logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke anayedaiwa kumuua bintiye wa miaka 2 na kula viungo vyake kuzuiliwa kwa siku 10

Naserian anatarajiwa kuhudhuria kesi hiyo Mei 8.

image
na Radio Jambo

Habari25 April 2023 - 10:02

Muhtasari


  • Wakati huo huo, mabaki ya bintiye yalihamishiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali kuu ya Kitengela.

Mahakama ya Kajiado imeamuru kuzuiliwa kwa mwanamke anayekabiliwa na shtaka la mauaji baada ya kudaiwa kumuua bintiye wa miaka miwili kwa kumkata vipande vipande kwa kisu na kisha kula sehemu za viungo vyake vya ndani.

Olivia Naserian anadaiwa kumuua bintiye Glory Njeri nyumbani kwao Kitengela eneo la Milimani Estate siku ya Jumapili, kisha kumlaza ndani kabla ya majirani kuwaarifu polisi, ambao walifika eneo la tukio na kumkamata.

Alifikishwa mbele ya Hakimu Mkuu Jane Kamau Jumanne ambaye aliamuru Naserian abaki rumande ya polisi kwa siku 10 nyingine ili kuruhusu maafisa wa polisi kukamilisha uchunguzi wao.

Naserian anatarajiwa kuhudhuria kesi hiyo Mei 8.

Wakati huo huo, mabaki ya bintiye yalihamishiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali kuu ya Kitengela.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved