logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanasha Donna atathmini kuhama Kenya akidai ni taifa la fujo tupu

Msanii huyo alisema kwamba mama yake anaishi Ubelgiji.

image
na Radio Jambo

Habari02 May 2023 - 12:00

Muhtasari


• Awali Donna amewahi nukuliwa akisimulia kwa kina kuhusu familia yake ambayo haijulikani na wengi.

Aliyekuwa mtangazaji na mzazi mwenziwe wa Diamond Platnumz, Tanasha Donna amedokeza kukosa furaha nchini Kenya na anatathmini kuhama kwenda mataifa ya nje pamoja na mtoto wake kabisa wasiweze kurejea tena.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Donna ambaye ni mama wa mtoto mmoja alilalamika kwamba mwaka huu tangu uanze nchi inasonga mbele vizuri katika mambo mengine lakini kila mara lazima kuna kitu hasi ambacho kitatokea.

Alisema kuwa anaendelea mchakato wa kukusanya kila kilicho chake akiwemo mtoto wake na kuhama kabisa, bila kutaja atakwenda taifa gani.

“Sitaki kudanganya, taifa hili ni fujo tupu. Ninajaribu kukusanya kile kilicho change pamoja na mwanangu na mizigo yangu na kuondoka kabisa tena kwa uzuri. Ni fujo tupu kwa sababu huwa tunasonga ndio lakini sasa kila siku tangu 2023 ianze lazima kuna kitu kibaya kitatokea. Kenya ni nini kinaendelea?” Tanasha Donna aliuliza.

Awali Donna amewahi nukuliwa akisimulia kwa kina kuhusu familia yake ambayo haijulikani na wengi.

Msanii huyo alisema kwamba mama yake anaishi Ubelgiji.

Mama huyo wa mtoto mmoja alizaliwa nchini Uingereza kwa baba wa Kiitaliano na mama Mkenya, lakini baadaye alihamia Kenya, ambako alikaa kwa muda kabla ya kuhamia Ubelgiji, ambako alilelewa na baba yake wa kambo kutoka Ubelgiji.

“Watu wanaponiuliza ninatoka wapi, sijui nianzie wapi. Nilizaliwa Uingereza, nilikulia Kenya kisha nikahamia Ubelgiji, lakini baba yangu mzazi ni Muitaliano na baadhi ya mchanganyiko huko, lakini nilikua na baba wa kambo wa Ubelgiji," aliandika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved