logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Messi aomba radhi kwa kusafari Saudi Arabia bila idhini

Nahodha huyo wa Argentina alisimamishwa na klabu hiyo kwa wiki mbili kwa ajili ya safari hiyo.

image
na Radio Jambo

Habari06 May 2023 - 12:51

Muhtasari


  • Messi anakaribia kuondoka PSG mkataba wake utakapomalizika majira ya joto.

Lionel Messi amewaomba radhi wachezaji wenzake wa klabu ya Paris St-Germain na kusema kuwa atasubiri klabu hiyo kuamua hatua itakayochukua dhidi yake baada ya kufanya safari bila kibali nchini Saudi Arabia.

Nahodha huyo wa Argentina alisimamishwa na klabu hiyo kwa wiki mbili kwa ajili ya safari hiyo.

Ilifuatia PSG kushindwa nyumbani na Lorient siku ya Jumapili - la tatu katika mechi sita - wakati Messi alicheza dakika 90.

"Naomba radhi kwa nilichofanya na nasubiri kuona klabu itaamua nini," Messi alisema kwenye video iliyowekwa kwenye mtandao wa Instagram.

"Kwa kweli nilifikiri tungekuwa na siku ya mapumziko baada ya mechi kama ilivyokuwa wiki zilizopita.

"Nilikuwa nimepanga safari hii kwenda Saudi Arabia baada ya kuighairi hapo awali. Wakati huu sikuweza kuighairi."

Messi anakaribia kuondoka PSG mkataba wake utakapomalizika majira ya joto.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35, ambaye pia amepigwa faini na klabu hiyo, ana jukumu la kuwa balozi wa utalii wa Saudi Arabia.

Meneja wa PSG Christophe Galtier anasema "hakuwa na uhusiano wowote na" kusimamishwa kwa Messi, huku pia akilaani maandamano ya mashabiki nje ya nyumba za wachezaji.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved