logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alinitongoza nikamwambia 'rent' yangu inaisha akatoroka bila kuangalia nyuma - Mrembo alia

"Nilimwambia tu sikumwomba alipie," mrembo huyo alitweet.

image
na Radio Jambo

Habari08 May 2023 - 08:39

Muhtasari


• Kulingana naye, alimwambia kwamba kodi ya nyumba yake ingeisha mwezi huo, na baada ya ufichuzi huo, aliacha tu kuzungumza naye na kuchimba mitini.

Mwanamke alia jamaa kumzimia data baada ya kumtongoza

Mwanamke mmoja ameshiriki na jamii nzima ya mtandao wa Twitter jinsi mvulana mmoja alivyomzimia bando chini ya saa 24 baada ya kumchumbia kwa sababu tu ya suala la kibinafsi alilomweleza kulihusu.

Akitambulishwa kama Josephine kwenye Twitter, mwanadada huyo alisema baada ya mwanamume huyo kumtupia ndoana, walikutana siku iliyofuata ili kufahamiana zaidi na ndipo walipozungumza kuhusu masuala yake ya kodi.

Kulingana naye, alimwambia kwamba kodi ya nyumba yake ingeisha mwezi huo, na baada ya ufichuzi huo, aliacha tu kuzungumza naye na kuchimba mitini.

Alibainisha kuwa hakuwahi kumwomba amlipie kodi hiyo bali alikuwa anamfahamisha tu hivyo ilishangaza kwamba aliamua kumzimia taa kutokana na kile alichokisema.

"Nilikutana na huyu jamaa jana tulizungumza nilimwambia kodi ya nyumba yangu itaisha mwezi huu na baba akaacha kuniongelesha, nilimwambia tu sikumwomba alipie," mrembo huyo alitweet.

Katika taarifa nyingine za kustaajabisha zilizosambazwa hapo awali kwenye mtandao wa Radio Jambo, mwanamume mmoja ameamua kusitisha harusi yake kama ilivyotokana na chapisho lililosambazwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya kugundua jambo lisilo la kawaida kuhusu mke mtarajiwa wake.

Mwanadada huyo ndiye aliyepeleka mitandaoni akilia kwamba bwana harusi mtarajiwa alisitisha mipango yote ya harusi baada ya kugundua kwamab alikuwa amemtembelea mpenzi wake wa zamani na hata kushiriki tendo la ndoa naye usiku wote, kwa kisingizio kwamba alikuwa amempelekea kadi ya mwaliko kuhudhuria harusi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved