logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Drake: Kwa nini nahisi asili yangu ni kutoka Nigeria

Pia iliorodhesha kuwa ana uhusiano na Cameroon, Congo, Ivory Coast na nchi nyingine za Afrika.

image
na Radio Jambo

Habari08 May 2023 - 12:40

Muhtasari


• Msanii huyo alisema kuwa matokeo hayo ni kutokana na usuli wa babake ambaye amekuwa akisimuliwa kuwa alikuwa Mwafrika.

Rapper wa Kanada, Drake amefunguka kwanini anadhani yeye ni Mnigeria.

Rapa, mtunzi wa nyimbo na mwigizaji aliyeshinda tuzo nyingi Drake, kwenye chapisho kwenye mtandao wake wa kijamii Jumatatu, Mei 8, 2023, alifichua kwa nini anadhani yeye ni Mnigeria.

Mwimbaji huyo anayetumia tovuti ya Ancestry.com aligundua kwamba alikuwa na uhusiano na Afrika kupitia baba yake Dennis Graham, lakini asilimia kubwa zaidi walikuwa wametoka Nigeria.

Rapa huyo aliweka picha ya matokeo yake kwenye tovuti ambayo pia iliorodhesha kuwa ana uhusiano na Cameroon, Congo, Ivory Coast na nchi nyingine za Afrika.

Rapa huyo alijibu ugunduzi huu na chapisho lililosomeka:

'Haya ni matokeo ya baba yangu. Je, hii inamaanisha mimi ni mwanamume wa Naija hatimaye?'

 

Mwezi mmoja uliopita, rapa huyo wa Kanada alitangaza bei mpya za kurekodi kwenye studio yake ya nyumbani huko Kanada ambapo msanii atahitaji kuzama mfukoni na kutengana na kitita cha milioni 33 za Kenya ili kurekodi kwa lisaa limoja tu.

Studio hiyo iko nyumbani kwake huko Kanada Toronto na ina vifaa vyote anavyotumia Drake. Katika Tweet hapo awali, Stufinder walisema kwamba "tunafahamu studio ya nyumbani ya Drake iliyoorodheshwa kwenye App yetu. Kwa sasa tunathibitisha kwamba Drake au timu yake walishiriki katika orodha hiyo."

Drake si msanii wa kwanza wa kigeni kufunguka wazi kuhusu chembechembe zake za Kiafrika kwani mwaka 2020 wakati wa vurugu za Donald Trump huko Marekani, wasanii mbalimbali walianza kujitenga na nchi hiyo kila mmoja akitafuta mizizi yake Afrika.

Msanii Card B alisema kuwa yeye angekuja Afrika angehamia Nigeria kama taifa la usuli wake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved