logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge wa zamani mwenye miaka 80 afunga harusi ya 9 na mrembo wa miaka 27

Mwanasiasa huyo mkongwe aliwahi kuwa mbunge kati ya 1992 na 2000.

image
na Radio Jambo

Habari10 May 2023 - 13:23

Muhtasari


• Picha za ndoa za kitamaduni za wanandoa zinaonyesha jinsi walivyo na furaha wanapochukua hatua hii.

• Tayari wanapanga fungate yao, ambayo itafanyika Ulaya.

Dominic Fobih na mke wake mpya.

Mbunge wa zamani wa nchini Ghana mwenye umri wa miaka 80 ameripotiwa kufunfa harusi yake ya tisa na mrembo mwenye umri wa miaka 27.

Kulingana na taarifa za vyombo vya habari nchini humo, Dominic Fobih alifunga ndoa yake ya 9 na mrembo mnamo Mei 7 mwaka huu.

Harusi ilifanyika katika nyumba ya familia ya bibi harusi katika Mkoa wa Ashanti nchini Ghana.

Fobih alikuwa amevalia nguo ya kitamaduni ya Kente, huku mke wake mpya akiwa amevalia gauni la corset nyeupe na yenye shanga za dhahabu, jariba moja liliripoti.

Picha za ndoa za kitamaduni za wanandoa zinaonyesha jinsi walivyo na furaha wanapochukua hatua hii.

Kulingana na taarifa, Mwanasiasa huyo alikuwa akijawa na majivuno alipokuwa akipiga picha na mke wake mpya, ambaye alionekana kustaajabisha akiwa amevalia gauni lake la harusi.

Fobih ni Waziri wa zamani wa Elimu na mwanachama wa National Democratic Congress (NDC). Aliwahi kuwa mbunge wa Assin Kusini kuanzia 1992 hadi 2000. Pia ni Waziri wa zamani wa Nchi katika Wizara ya Elimu.

Hii ni ndoa ya tisa ya Fobih. Ameoa mara nane hapo awali, na amezaa watoto 18. Ndoa zake za awali zimeisha kwa talaka.

Ndoa ya hivi punde ya Fobih imekumbwa na maoni tofauti kutoka kwa Waghana. Baadhi ya watu wamempongeza kwa kupata mapenzi, huku wengine wakimkosoa kwa kuoa mwanamke ambaye ni mdogo sana kwake.

Bila kujali maoni ya umma, Fobih na mke wake mpya wanaonekana kuwa na furaha sana pamoja. Tayari wanapanga fungate yao, ambayo itafanyika Ulaya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved