logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wafahamu Wakenya mashuhuri waliosali katika ukuta wa Jerusalem

Mwaka wa 2016, rais mstaafu Uhuru Kenyatta alifanya ziara ya kutembelea ukuta huo ambapo alifanya maombi.

image
na Radio Jambo

Habari11 May 2023 - 09:14

Muhtasari


•Katika picha zilizosambazwa siku za Jumatano, rais na mkewe walionekana wakiinama kwa maombi katika eneo hilo.

•Mwaka wa 2016, rais mstaafu Uhuru Kenyatta alifanya ziara ya kutembelea ukuta huo ambapo alifanya maombi.

mashuhuri waliosali katika ukuta wa Jerusalem

Rais William Ruto na mkewe Rachel Ruto walitembelea Ukuta wa Wailing Wall mjini Jerusalem  wakati wa ziara yake nchini Israel.

Katika picha zilizosambazwa siku za Jumatano, rais na mkewe walionekana wakiinama kwa maombi katika eneo hilo.

Eneo hilo lililo katika jiji la kale la Jerusalemu ni ukuta wa mwisho uliobaki wa nje wa hekalu la kale la Kiyahudi na ni eneo muhimu sana la historia ya kisasa ya Israeli. Ni bure kwa kila mtu  na iko wazi masaa 24.

Rais na mkewe sio Wakenya wa kwanza  kuwahi kufanya maombi mbele ya ukuta huo.

Mwaka wa 2016, rais mstaafu Uhuru Kenyatta alifanya ziara ya kutembelea ukuta huo ambapo alifanya maombi.

Kiongozi wa Azimio-One Kenya, Raila Odinga alifika katika eneo hilo mwaka wa 2017 ambapo aliomba.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved