logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mahakama yatupilia mbali ombi la Ezekiel la kurejeshewa akaunti za benki

Mahakama imetupilia mbali ombi la Mchungaji Ezekiel la kutaka akaunti zake za benki zisifungwe.

image
na

Habari15 May 2023 - 09:55

Muhtasari


•  Jaji Sawe Alisema ataepuka kutoa maoni yake kuhusu usahihi na uhalali wa maagizo yaliyotolewa na Mahakama ya Nairobi wiki jana.

• Odero aliwasilisha ombi lake katika Mahakama Kuu ya Mombasa mnamo Mei 3 akiomba amri ya serikali kufungia zaidi ya akaunti 15 za kibinafsi na za kanisa.

Mchungaji Ezekiel Odero mahakamani.

Mahakama kuu ya Mombasa imetupilia mbali ombi la Mchungaji Ezekiel Odero la kutaka akaunti zake zaidi ya 15 za benki zisifungwe.

Jaji wa Mahakama Kuu Olga Sewe alisema ombi hilo ni potofu na haliwezi kutekelezeka.

Alisema ataepuka kutoa maoni yake kuhusu usahihi na uhalali wa maagizo yaliyotolewa na Mahakama ya Nairobi wiki jana.

Mahakama Kuu pia ilitupilia mbali ombi la maagizo yaliyotaka leseni ya TV yake kerejeshwa, ikisema walalamishi walipaswa kutumia njia zote za kisheria na Mamlaka ya Mawasiliano kabla ya kufika mahakamani.

Odero aliwasilisha ombi lake katika Mahakama Kuu ya Mombasa mnamo Mei 3 akiomba amri ya serikali kufungia zaidi ya akaunti 15 za kibinafsi na za kanisa.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved