logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Urusi na Ukraine: Mji wa Kyiv waamkia mashambulizi makali kutoka kwa Urusi

Meya wa jiji Vitali Klitschko alisema baadhi ya vifusi vya roketi vimeanguka katika wilaya za kati.

image
na Radio Jambo

Habari16 May 2023 - 07:38

Muhtasari


•      Jumbe za serikali zilionya watu kujiepusha na madirisha huku vifusi vya makombora yaliyozuiwa vikianguka kutoka angani.

Mshambuliai ya Urusi Kyiv

Kuna ripoti za idadi kubwa ya milipuko katika mji mkuu wa Ukraine, Kyiv, na ving'ora vya mashambulizi ya anga vimekuwa vikilia.

Katika video kwenye mitandao ya kijamii, mifumo ya ulinzi wa anga inaweza kuonekana ikirusha makombora yanayoshukiwa kuwa ya Kirusi.

Jumbe za serikali zilionya watu kujiepusha na madirisha huku vifusi vya makombora yaliyozuiwa vikianguka kutoka angani.

Meya wa jiji Vitali Klitschko alisema baadhi ya vifusi vya roketi vimeanguka katika wilaya za kati, ikiwa ni pamoja na bustani ya wanyama ya jiji.

Kuna ripoti za majeruhi.

Shambulio hilo tata, ambalo lilitumia ndege zisizo na rubani na makombora, lilielezewa kuwa "la kipekee katika msongamano wake" na afisa mmoja wa Kyiv.

Serhiy Popko, mkuu wa utawala wa kijeshi wa mji mkuu wa Ukraine, alielezea shambulio hilo kuwa na "idadi ya juu zaidi ya makombora ya mashambulizi katika kipindi kifupi zaidi cha muda".

"Kulingana na taarifa za awali, idadi kubwa ya malengo ya adui katika anga ya Kyiv yaligunduliwa na kuharibiwa," aliongeza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved