logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Whatsapp yakubali watumizi kuficha jumbe za siri

Whatsap kuwaruhusu wateja kuzificha jumbe zao za kibinafsi.

image
na

Habari16 May 2023 - 06:10

Muhtasari


• Mabadiliko haya yalitangazwa na mmiliki wa mtandao huo Mack Zuckerberg katika akaunti yake ya facebook.

• Mabadiliko haya yatawaruhusu watumiaji wa whatsapp kuweza kuzificha jumbe ambazo hawataki kujulikana kwenye folda yenye neno siri.

Kampuni ya mawasalinao ya Whatsapp imefanya mabadiliko na sasa unaweza kumkabali mtu kuficha mazungumzo au jumbe.

Mabadiliko haya yatawaruhusu watumiaji wa whatsapp kuzificha jumbe ambazo hawataki kujulikana kwenye folda yenye neno siri.

Mfuko huo wa siri hautaonyesha notisi ya ujumbe kuingia kama ilivyo kawaida ya jumbe za kawaida ili kuarifu mtumiaji kuwa kuna ujumbe mpya.

Mabadiliko haya yalitangazwa na mmiliki wa mtandao huo Mack Zuckerberg katika akaunti yake ya facebook.

Mabadiliko haya yanajiri baada ya mabadiliko kadhaa kutangazwa na Zuckerbarg hivi majuzi.

Pia mtandao huo pia sasa unawaruhusu watumiaji kuchapisha sauti katika status zao za whatsapp.

Watumiaji pia wanaweza kutoa hisia zao badala ya kuandika majibu (kulia, kicheko, kulia, kupenda moyo, kushtuka na kuomba).


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved