logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mike Sonko kumsadia mwanamke aliyekamatwa na polisi baada ya kuharibu mali ya mchumba wake

Mike Sonko amejitolea kusaidia mwanamke anayeshukiwa kuharibu mali ya mchumba wake.

image
na

Habari19 May 2023 - 07:25

Muhtasari


• Mwanamke huyo anadaiwa kuharibu gari la mpenzi wake na kuvunja runinga yake alipompata mpenzi wake akiwa kwenye tendo hilo.

• Mike Sonko alichapisha kwenye akaunti yake ya Twitter kuashiria kutorithika na umauzi huo wa mahakama kuhusu suala hilo.

Sonko aonesha kiburi cha pesa Twitter

Mike Sonko amejitolea kusaidia mwanamke anayeshukiwa kuharibu mali ya mchumba wake.  

Mwanamke huyo kwa jina Imelda Mwendwa Kiguda alikamatwa Jumatatu kwa madai ya kuharibu mali ya mpenzi wake baada ya kumfumania na mwanamke mwingine.

Mwanamke huyo anadaiwa kuharibu gari la mpenzi wake na kuvunja runinga yake alipompata mpenzi wake akiwa kwenye tendo hilo.

Alipofikishwa kortini binti huyo alitakiwa kulipa dhamana ya pesa taslimu sh100,000.

Mike Sonko alichapisha kwenye akaunti yake ya Twitter kuashiria kutorithika na umauzi huo wa mahakama kuhusu suala hilo.

Katika ujumbe wake Twitter, Sonko alijitolea kulipa dhamana ya pesa taslimu na kuwaomba marafiki na familia ya mwanamke huyo kumtuma  nambari ya kesi hiyo mara moja.

"Hili halikubaliki kabisa, hebu marafiki na jamaa wa bibi huyu nitumie namba ya kesi mahakamani mara moja ili nimdhamini." sonko aliandika.

Sonko pia alisema kuwa atamlipa wakili yeyeto atakaye jitokeza na kumwakilisha mwanamke huyo kotini.

"Alafu, wakili yeyeto mwanamke achukue kesi hio na kumtetea huyu binti nitalipa malipo ya kisheria kwa niaba yake." Sonko aliongeza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved