logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume apatikana ameuawa Mlolongo kaunti ya Machakos

Alisema mwili huo ulikuwa na majeraha yanayoonekana.

image
na

Habari19 May 2023 - 10:09

Muhtasari


  • Maafisa wa upelelezi wa DCI kutoka kituo cha polisi cha Mlolongo wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.

Mwanamume mmoja amepatikana ameuawa  Mlolongo, kaunti ya Machakos.

Mwili wa mwanamume huyo mwenye umri wa kati ya miaka 25 na 30, ulipatikana ukiwa karibu na kanisa la ABC kando ya barabara ya Makanisa ndani ya Kitongoji cha Mlolongo huko Athi River Mashariki siku ya Ijumaa.

Mwanamume huyo anashukiwa kuuawa kwa muda usiojulikana Alhamisi usiku.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Athi River Mashariki Anderson Njagi alisema eneo la tukio lilikuwa limeshughulikiwa na mwili huo kuhamishiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.

"Marehemu ni mtu anayejulikana sana, mkulima huko Lukenya," Njagi aliambia Radiojambo kwenye simu.

Alisema mwili huo ulikuwa na majeraha yanayoonekana.

Kulingana na duru za habari ni kuwa marehemu alitambuliwa na mmoja wa ndugu zake.

Kesi hiyo iliripotiwa katika kituo cha polisi cha Mlolongo kama ripoti ya tukio la kifo cha Mei 19.

Mwili wa marehemu ulihamishwa hadi katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Machakos Level 5 ukisubiri kufanyiwa uchunguzi.

Maafisa wa upelelezi wa DCI kutoka kituo cha polisi cha Mlolongo wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved