logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uteuzi wa Kenya kwanza ndio mwanzo wa ufisadi-Seneta Osotsi

Seneta huyo alimtaka rais kuangalia umahiri wa wafanyikazi anaowateua serikalini.

image
na Radio Jambo

Habari22 May 2023 - 09:38

Muhtasari


  • Seneta huyo aliendelea kudai kuwa uteuzi unaofanywa na serikali haulengi kuwasilisha maswala ya kimsingi yanayoathiri wananchi bali wale walioteuliwa kulipwa.

Seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi amedai kuwa uteuzi uliofanywa na serikali ya Kenya Kwanza unachochea ufisadi.

Katika mahojiano katika kipindi cha DayBreak cha runinga ya Citizen mnamo Jumatatu, Seneta huyo alitoa maoni kuwa baadhi ya watu wanaodaiwa kuhusika katika sakata hiyo ya sukari wanafanya kazi kwa karibu na rais.

"Baadhi ya watu wanaodaiwa kuhusika katika sakata hii ya sukari na hata KEMSA walikuwa wameketi nyuma yake," alisema Osotsi.

Seneta huyo aliendelea kudai kuwa uteuzi unaofanywa na serikali haulengi kuwasilisha maswala ya kimsingi yanayoathiri wananchi bali wale walioteuliwa kulipwa.

"Hawa watu hawapangiwi huko kwenda kufanya kazi na kutoa, wanateuliwa huko kwenda kufanya kazi na kupata," alisema.

Katika kueleza jinsi maafisa wanavyojipanga kupata pesa kupitia ufisadi, alitoa mfano wa wajumbe wa bodi ambao kulingana naye wanastahili kupata takriban Ksh.320,000 kwa mwaka lakini wakaishia kuchuma zaidi.

Alitaja utoaji wa zabuni na ajira kuwa ni maeneo ambayo kuna rushwa na kwamba wajumbe wa bodi huwatumia maafisa wa kiufundi ili kuwezesha rushwa.

Seneta huyo alimtaka rais kuangalia umahiri wa wafanyikazi anaowateua serikalini.

"Kwa yeye kuwa makini na vita dhidi ya rushwa, nadhani inaanza na ubora, uwezo, umahiri na tabia za watu wanaoteuliwa," alibainisha.

Osotsi aliendelea kusema kuwa historia ya ufisadi ya mtu ni muhimu katika kubainisha uteuzi.

Aliongeza kuwa mtu anayekabiliwa na kesi za ufisadi hapaswi kuzingatiwa kazi za serikali isipokuwa kesi hizo zimefutwa kortini.

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved