logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Brighton yawapa wachezaji, wafanyikazi nyongeza ya 20% kwa kufuzu ligi ya Uropa

Kando na wachezaji, uongozi wa timu hiyo utawapa nyongeza wafanyikazi zaidi ya 1000.

image
na Radio Jambo

Habari24 May 2023 - 09:37

Muhtasari


• Brighton watamenyana na mabingwa wa ligi ya premia Manchester City katika mchezo wao wa pili kuelekea mwisho wa kampeni Jumatano.

• Klabu ya Brighton haiwezi kumaliza chini ya nafasi ya saba kama ilivyo, ambayo ingewafanya kufuzu kwa Ligi ya Konferensi ikiwa ndivyo ilivyokuwa.

Uongozi wa Brighton kuwapa wachezaji nyongeza ya misharaha kwa asilimia 20.

Wachezaji na wafanyikazi wa timu ya Brighton wanaripotiwa kupokea bonasi ya asilimia 20 baada ya Seagulls kufuzu kwa mashindano ya Uropa kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Kikosi cha Roberto De Zerbi karibu kitamaliza katika nafasi ya sita na kuwa kwenye Ligi ya Europa muhula ujao kutokana na tofauti yao ya mabao kuwa bora zaidi ya Aston Villa lakini wanahitaji pointi moja zaidi ili kuondoa uwezekano wowote wa kuteleza kwenye Ligi ya Europa Conference.

Kuthibitishwa kwa soka la Ulaya msimu ujao kumepelekea mmiliki wa klabu, Tony Bloom, kuwazawadia zaidi ya wafanyakazi 1,000 na nyongeza ya asilimia 20 ya mshahara wa kila mwaka kutokana na mafanikio hayo makubwa, kulingana na The Times.

Brighton watamenyana na mabingwa wa ligi ya premia Manchester City katika mchezo wao wa pili kuelekea mwisho wa kampeni Jumatano kabla ya kumenyana na Aston Villa siku ya mwisho.

Villa ndio, kimahesabu, timu pekee inayoweza kuruka Brighton kwenye jedwali lakini kikosi cha Unai Emery kingehitaji mabadiliko makubwa katika tofauti ya mabao ili kuteleza hadi nambari saba.

Klabu ya Brighton haiwezi kumaliza chini ya nafasi ya saba kama ilivyo, ambayo ingewafanya kufuzu kwa Ligi ya Konferensi ikiwa ndivyo ilivyokuwa.

Bloom aliwahutubia wachezaji katika Amex siku ya Jumapili, akisema: 'Nimekuwa nikiisaidia klabu hii kwa miaka 45 na singewahi kufikiria hali hii ambapo tunashindana dhidi ya timu bora zaidi duniani.

'Ina maana sana kwangu, kwa mashabiki wetu, kwa jiji, na mmeweka mengi katika msimu.

 

'Mtazamo wenu, ustadi wenu, kuimarika tulipokuwa na matokeo mabaya, jambo ambalo halijatokea mara kwa mara, tulirudi kwa nguvu sana katika mchezo unaofuata na ninajivunia kila mmoja wenu.'


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved