logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zakayo Mtoza ushuru – Rais Ruto akubali jina jipya la majazi

Rais Ruto aliahidi kuangazia kuwepo kwa siku ya wakusanyaji ushuru.

image
na

Habari26 May 2023 - 07:47

Muhtasari


•Tunayo siku ya watoa ushuru,pendekezo langu ni kuwa,tunaweza kuwa na siku ya wakusanyaji ushuru labda katika ikulu.

•Kwa kuwa nimerejelewa kama Zakayo katika baadhi ya maeneo,hili ni pendekezo zuri na tutaliangazia

Rais William Ruto

Rais William Ruto amekiri kwamba tayari raia wamembandika jina Zakayo mtoza ushuru.

Hili limebainika katika jumba la Times Tower alipokuwa akizungumzia  kuhusu namna  ya kuendesha taifa mbele kutokana na ushuru.Ruto alipokuwa akihutubia umati, alilisema hilo alipoulizwa iwapo kuna uwezekano wa kuwepo kwa siku ya wakusanyaji ushuru swali lilioulizwa na mmoja wa maafisa wa KRA.

“Tunayo siku ya watoa ushuru,pendekezo langu ni kuwa,tunaweza kuwa na siku ya wakusanyaji ushuru labda katika ikulu?” Muila aliuliza.

Ruto alimjibu kuwa, tayari amekwisha kuwekwa jina Zakayo katika baadhi ya maeneo, hilo ni pendekezo zuri na hivyo serikali italitilia maanani.

“Kwa kuwa nimebandikwa jina Zakayo katika baadhi ya maeneo,hili ni pendekezo zuri na tutaliangazia.”Ruto alimjibu.

“Tutaendelea kutafuta  njia ambazo ushuru utakusanywa kwa uadilifu kuhakikisha hakuna kuvuja.” Rais aliendelea.

Haya yanajiri huku wakenya wakipitia hali ngumu ya maisha kutokana na bei ghali ya bidhaa muhimu za matumizi. Shirika la mafuta nchini limekuwa la punde kutangaza kupandishwa kwa bidhaa hiyo huku nayo kampuni ya  umeme na kawi ikiendelea  kupandisha bei ya huduma hizo bila kuzungumzia bei ya sukali ambayo kwa sasa ni maradufu.

Rais ambaye anapigia debe kuwepo kwa ushuru ili kufanikisha ujenzi wa nyumba, alieleza bayana kuwa nia yake ni kuhakikisha wakenya wapepata makao mazuri tena ya bei nafuu ili wanaoishi vibandani pia wanufaike.

Ruto pia aliendelea na kusema kwamba, cha muhimu ni kuhakikisha kwamba ushuru unaotozwa wananchi unatumika kwa njia ambayo inakusudiwa na ataendeleza uwazi kuukomesha ufisadi na uvujaji wa mali ya umma na hivyo Wakenya wamwuunge mkono.

“Itatarajiwa kuwa gharama ya maisha itakuwa juu,maana nasikia sina pesa ya za kununua baadhi ya bidhaa,lakini licha ya hayo lazima pia taifa lisonge mbele.Hili litafanyika kupitia ushuru kutoka kwetu sisi Wakenya.” Ruto alieleza hoja ya teknolojia katika taifa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved