logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DP Gachagua awapa wanafunzi wa St Charles Lwanga Sh500,000 za 'lunch'

Gachagua pia aliahidi kuwanunulia wanafunzi basi la shule.

image
na

Habari03 June 2023 - 13:56

Muhtasari


•“Sasa mimi naona tufanye ile mambo ya chakula cha mchana, nitampa mkuu wa shule Sh500,000 kwa ajili ya chakula cha mchana,” Gachagua alisema.

•Gachagua pia alihoji ni kwa nini kiongozi wa Azimio Raila Odinga hakuhudhuria Harambee akisema Kitui ni ngome ya Raila.

akiwa na wanafunzi wa St Charles Lwanga katika Kaunti ya Kitui mnamo Juni 3, 2023

Naibu Rais Rigathi Gachagua ametoa Sh500,000 kwa shule ya St Charles Lwanga, Kitui.

DP alikuwa ameenda shuleni humo kwa harambee kwa ajili ya maendeleo.

“Sasa mimi naona tufanye ile mambo ya chakula cha mchana, nitampa mkuu wa shule Sh500,000 kwa ajili ya chakula cha mchana,” alisema.

"Si mkikula chapati ni sawa, na soda."

Gachagua pia aliahidi kuwanunulia wanafunzi basi la shule.

“Mimi sijawahi sikia viongozi wenu wamenunua basi la shule, sasa naona Scania itaweza,” alisema.

Alisema ni muhimu kuweka fedha za kutosha katika shule hiyo ili kuimarisha maendeleo yake na kuwapa wanafunzi mazingira mazuri ya kujifunzia.

"Sisi ni watu wa kazi, siasa imeisha tuko tayari kufanya kazi," alisema.

Gachagua pia alihoji ni kwa nini kiongozi wa Azimio Raila Odinga hakuhudhuria Harambee akisema Kitui ni ngome ya Raila.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved