logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Otile Brown atengana na meneja wake baada ya miaka sita

Mwanamziki Otile Brown na meneja wake wametangana baada kufanya kazi pamoja kuanzia mwaka wa 2017.

image
na

Habari07 June 2023 - 05:02

Muhtasari


Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyochapishwa kwenye akaunti yake ya Instagram siku ya Jumanne, Otile aliangaza habari za kutengana kwao.

Otile aliwahakikishia mashabiki wake kwamba licha ya kuachana na Noriega, ataendelea kufanya muziki wake.

Otile Brown na Meneja wake Joseph Noriega.

Mwanamziki Jackob Obunga almaarufu Otile Brown wametengana na meneja wake Joseph Noriega baada kufanya kazi pamoja kuanzia mwaka wa 2017 na kupata mafanikio mengi kimziki.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyochapishwa kwenye akaunti yake ya Instagram siku ya Jumanne, Otile alitangaza habari za kutengana kwao, akitaja wakati wao pamoja kama "Safari ya Ajabu".

Otile alitoa shukrani kwa Noriega kwa jukumu lake kubwa la kumtengeneza kama msanii katika safari yake yote ya muziki.

"@noriega_donself barikiwa mfalme, nakupenda daima. Asante kwa safari, kumbukumbu zote na mafanikio tuliyoyapaa aia safari hii ya muziki . Nimefurahishwa na kile kitakachotokea mbeleni, "Brown aliandika.

Noriega kwa upande wake alimshukuru Otile Brown kwa kumbukumbu na mafanikio  waliopata pamoja.

“Nashukuru kwa safari, Kumbukumbu na mafanikio yetu pamoja…..Mungu akubariki,” Noriega alisema.

Otile aliwahakikishia mashabiki wake kwamba licha ya kuachana na Noriega, ataendelea kufanya muziki wake.

"Ingawa Noriega atakosekana, Otile Brown anaendelea kujitolea kwa safari yake ya muziki kwa ari na ari sawa. Mashabiki wanaweza kuwa na uhakika kwamba maono ya Brown na muziki wa kipekee utaendelea,” ilisoma taarifa kutoka kwa lebo ya mwimbaji huyo, Just In Love Music.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved