logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Haaland atarajiwa kuongoza City kushambulia Inter Juni 10

Amefunga mabao 52 katika mashindano yote huku 36 akifunga kwenye ligi ya Premier

image
na

Habari09 June 2023 - 10:08

Muhtasari


• Haaland, kwa mechi 52 katika mashindano yote, ameweza kufunga mabao 52 huku 36 akiyafunga kwenye ligi ya Premier.

• Historia ya vijana hao wa Pep kutolinyakua taji la EUFA licha ya kufika fainali msimu wa 2021, itabadilika iwapo watapata ushindi dhidi ya Inter Milan

Erling Haaland

Huku shindano la Ligi ya Mabingwa likitarajiwa kufika ukingoni msimu huu hapo kesho Juni 10,klabu ya Manchester City haijapoteza mechi yoyote katika shindano hilo msimu huu.

Kwa Mechi 12, City imecheza kufikia sasa kwenye shindano hilo, imepata ushindi mara saba na sare mara tano.

Mshambulizi Erling Haaland ndiye anayemulikwa sana na mashabiki wa kabumbu, kutokana na jinsi amekuwa akicheka na wavu msimu huu tangu ajiunge na vigogo hao wa soka Uingereza.

Haaland, kwa mechi 52 katika mashindano yote, ameweza kufunga mabao 52 huku 36 akiyafunga kwenye ligi ya Premier.

Nyota huyo mwenye uraia wa Norway ameifaa sana klabu ya City, tangu walipomsajili kutoka Borussia Dortmund msimu wa joto uliopita. Ameisadia City kulibeba taji la Premier pamoja na FA, huku akitarajiwa kuiweka historia mpya klabuni iwapo atalinyakua taji la Champions League Jumamosi hii mjini Istanbul.

Chini ya ukufunzi wa meneja Pep Guardiola, Man City wameshinda Premier League mara tano kwa misimu 6, jambo ambalo limeifanya klabu hilo kuorodheshwa kuwa miongoni mwa klabu bora ulimwenguni.

Historia ya vijana hao wa Pep kutolinyakua taji la EUFA licha ya kufika fainali msimu wa 2021, itabadilika iwapo watapata ushindi dhidi ya Inter Milan.

Licha ya hayo, Man City ina hofu kuwa huenda huenda kitumbua chao kikaingia mchanga, hasa wanapomshuku kiungo mkabaji Kyle Walker kuanza katika mechi hiyo ndipo amthibiti mshambulizi wa Argentina Lautaro Martinez.

Limebakia kuwa jambo la muda, kwa Haaland na City kuibadili historia, au mambo yataendelea kutumbukia nyongo hasa katika shindano la Champions League.

Unamtakia nani ushindi kati ya Man City na Inter Milan?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved