logo

NOW ON AIR

Listen in Live

N'Golo Kanté afeli vipimo vya afya katika azma ya kwenda Saudia kutoka Chelsea

"Kante alisaini makubaliano ya lazima, sio mkataba wa mwisho," chanzo kilinukuliwa na AFP.

image
na Radio Jambo

Habari09 June 2023 - 09:24

Muhtasari


• Siku ya Jumanne, klabu hiyo yenye makao yake mjini Jeddah ilimtambulisha rasmi mshindi wa tuzo ya Ballon d'Or ya Ufaransa Karim Benzema.

• Benzema na Kante wako kwenye orodha ya takriban walengwa 10 ambao wamewasiliana na maafisa wa Saudi.

N'golo Kante afeli afya katika azma ya kwenda Saudi Arabia.

Safari ya kiungo wa kati wa Chelsea, Mfaransa Ngolo Kante kuelekea Saudi Arabia kujiunga na timu ya Al Ittihad huenda italazimika kusubiriwa Zaidi baada ya taarifa za ndani kutoka kwa timu hiyo ya Saudia kufichua kwamba Mfaransa huyo alifeli katika vipimo vya afya.

Kulingana na jarida la AFP, Kante alikuwa amekubali mkataba wa kumweka Al Ittihad hadi mwaka 2026 lakini awamu ya mwisho na ambayo ni muhimu ya vipimo vya matibabu ikifeli.

Kante, 32, ana historia ya majeraha na alikosa miezi sita ya msimu wa Ligi Kuu ya Chelsea kutokana na tatizo la misuli ya paja.

Chanzo cha Al-Ittihad kilisema Kante alitia saini makubaliano ya lazima lakini klabu hiyo inachunguza matokeo ya vipimo vya afya kabla ya kukubaliana mkataba wa mwisho.

Siku ya Jumanne, klabu hiyo yenye makao yake mjini Jeddah ilimtambulisha rasmi mshindi wa tuzo ya Ballon d'Or ya Ufaransa Karim Benzema mwenye umri wa miaka 35 kama mchezaji mkubwa zaidi katika historia yao.

"Kante alisaini makubaliano ya lazima, sio mkataba wa mwisho," chanzo kilinukuliwa na AFP.

"Bado tunapitia matokeo ya uchunguzi wa afya. Ana historia ndefu ya majeraha na tunataka kuwa makini kabla ya kusaini mkataba mkubwa."

Usajili wa Benzema umekuja baada ya supastaa wa Ureno Cristiano Ronaldo kujiunga na Al-Nassr ya Saudi Arabia mwezi Januari kwa mkataba unaodaiwa kuwa wa zaidi ya euro milioni 400.

Benzema na Kante wako kwenye orodha ya takriban walengwa 10 ambao wamewasiliana na maafisa wa Saudi, chanzo kilicho karibu na mazungumzo hayo kiliiambia 'AFP' wiki iliyopita.

Mchezaji wa Argentina Lionel Messi alitangaza siku ya Jumatano kuwa amekataa kandarasi ya juu kabisa huko Saudi Arabia ili ajiunge na Inter Miami ya MLS.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved