logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi apewa kichapo cha mbwa koko msikitini kwa kupatikana na ng'ombe aliyeibwa

Hata hivyo polisi huyo aliokolewa na kupelekwa katika kituo cha polisi.

image
na Radio Jambo

Habari09 June 2023 - 09:00

Muhtasari


• Inaarifiwa kwamba afisa huyo aliviziwa na kuonekana akimshusha ng’ombe huyo wa wizi kutoka katika gari la polisi huku akimpeleka mtoni kunywa maji.

• Aliyemuona aliwaita wanakijiji ambao bila kusita walifika kwa makumi chini ya dakika chache kabla ya kuanza kumpakulia polisi huyo adhabu.

Polisi mmoja katika kaunti ya Kakamega alijipata pabaya kwenye mikono ya wananchi wenye ghadhabu baada ya wananchi hao kumfumania akiwa na ng’ombe aliyedhaniwa kuwa wa wizi.

Kulingana na Citizen, wananchi walijawa na ghadhabu baada ya kugundua kwamba ng’ombe ambaye alikuwa ametoweka kwa njia za utata kutoka  boma moja kijijini humo alikuwa mikononi mwa afisa wa polisi.

Baada ya kumkuta na ng’ombe huyo, wananchi walimuangushia kichapo cha mbwamwitu msikitini katika kile kiliripotiwa kuwa ni kumtuhumu afisa huyo wa polisi kutekeleza wizi kwa kutumia dola.

Inaarifiwa kwamba afisa huyo aliviziwa na kuonekana akimshusha ng’ombe huyo wa wizi kutoka katika gari la polisi huku akimpeleka mtoni kunywa maji.

Aliyemuona aliwaita wanakijiji ambao bila kusita walifika kwa makumi chini ya dakika chache kabla ya kuanza kumpakulia polisi huyo adhabu.

Walimpata polisi huyo akiosha gari hilo ili kuodnoa chembechembe za kinyesi ambacho mnyama huyo alikuwa amejisaidia kwenye gari hilo.

Polisi huyo alinusuriwa baadae na kupelekwa katika kituo cha polisi


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved