logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto amteua mkuu mpya wa mkutano wa Africa Climate Summit

Ataongoza jopo la ACS na kusimamia upangaji na uratibu wa shughuli zote.

image
na Radio Jambo

Habari09 June 2023 - 15:20

Muhtasari


  • GEAPP iliundwa ili kusaidia kuharakisha nishati safi kwa kila mtu, kila mahali, kwa watu na sayari.

Rais William Ruto Ijumaa alimteua Joseph Ng’ang’a kuwa Afisa Mkuu Mtendaji wa Mkutano wa Kilele wa Africa Climate Summit (ACS) utakaofanyika Septemba hapa Nairobi.

Bw. Ng’ang’a ni Makamu wa Rais wa Muungano wa Kimataifa wa Nishati kwa Watu na Sayari (GEAPP).

Ataongoza jopo la ACS na kusimamia upangaji na uratibu wa shughuli zote.

Bw. Ng’ang’a atafanya kazi kwa karibu na Waziri wa Mazingira Soipan Tuya na washikadau wengine.

GEAPP ni muungano wa hisani, serikali, teknolojia, sera na washirika wa ufadhili ulioanzishwa na The Rockefeller Foundation, IKEA Foundation, na Bezos Earth Fund.

GEAPP iliundwa ili kusaidia kuharakisha nishati safi kwa kila mtu, kila mahali, kwa watu na sayari.

Bw. Ng’ang’a pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafadhili wa Nishati Endelevu kwa Wote na mwanzilishi mwenza wa Africa Carbon Markets Initiative.

Mkutano wa kilele wa Afica Climate Summit utaandaliwa kwa pamoja na Kenya na Umoja wa Afrika mjini Nairobi kuanzia Septemba 4 hadi 6.

Bw Ng’ang’a alijiunga na Simon Harford, Mkurugenzi Mtendaji wa GEAPP, na William Asiko, Makamu wa Rais wa Rockefeller Foundation Africa, katika uzinduzi wake katika Ikulu ya Nairobi.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved