logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Omanyala ashindwa kunyakua dhahabu kwa mara nyingine tena ndani ya wiki moja

Mkenya huyo sasa atapumzika kwa wiki saba kabla ya kujiandaa kwa mashindano mengine Budapest.

image
na Radio Jambo

Habari10 June 2023 - 11:52

Muhtasari


• Mkenya huyo sasa atapumzika kwa wiki saba kabla ya kujiandaa kwa mashindano mengine Budapest.

akishiriki mashindano ya dunia huko Oregon

Kwa mara nyingine tena, mwanariadha wa mbio za mita mia moja Mkenya Ferdinand Omanyala ameshindwa kunyakua dhahabu katika mbio hizo kwenye mashindano ya Diamond League yaliyofanyika usiku wa Ijumaa jijini Paris Ufaransa.

Omanyala alimaliza wa pili kwa sekunde 9.98 nyuma ya bingwa wa dunia katika mbo za mita 200, Mmarekani Noah Lyles aliyeshinda dhahabu kwa kutimka sekunde 9.97, ikiwa ni tofauti na 0.01 tu.

Omanyala alionekana kupangiwa kushinda mbio za kwanza za Diamond League katika maisha yake ya soka, lakini Lyles aliongeza kasi akiwa na chini ya mita 30 kabla ya kushinda.

Mkali wa Botswana na Bingwa wa Dunia wa U-20 Letsile Tebogo alimaliza wa tatu kwa muda wa sekunde 10.05.

Hizo zilikuwa mbio za tatu kwa Omanyala katika Ligi ya Diamond mwaka huu baada ya kumaliza wa tatu mjini Rabat na wa pili katika Ligi ya Diamond ya Florence wiki jana.

Mbio hizo pia zilishuhudia kurudi kwa Bingwa wa Olimpiki Marcell Lamont Jacobs, ambaye aliruka pambano lake na Fred Kerley huko Rabat na Florence.

Muitaliano huyo, hata hivyo, alicheza vibaya alipomaliza nafasi ya 7.

Omanyala ambaye ni Bingwa wa Jumuiya ya Madola sasa atapumzika kwa wiki saba kutoka kwa mashindano ya kimataifa kujiandaa na Mashindano ya Riadha ya Dunia huko Budapest baadaye mwaka huu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved