logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mulamwah: Kwa sasa siko tayari kuwa na mwanamke juu niliachwa bila pesa

Mulamwah alisema kuwa Ruth K amesainiwa chini ya Mulamwah Entertainment.

image
na Radio Jambo

Habari29 June 2023 - 08:53

Muhtasari


• Mulamwah hata hivyo hakuweza kufutilia mbali kabisa uwezekano wa kuchumbiana na mrembo Ruth K akisema;

• “Yeye ni bestee kwa sasa, kwa hiyo kama vitu vingine vitakuwa pengine huko mbele mbele, huwezi jua,” alisema.

Mulamwah asema hataki wanawake sasa hivi.

Kwa mara nyingine tena, mchekeshaji wa mitandaoni Kendrick Mulamwah amenyoosha maelezo kuhusu rafiki yake wa Karibu Ruth K ambaye wanapenda kutaniana kwa msimbo ‘bestee bestee’ licha ya wengi kuhisi kuna kitu Zaidi ya urafiki wa kawaida.

Mulamwah ameweka wazi kwamba Ruth K atasalia kuwa rafiki yake wala hakuna kitu kinachondelea baina yao Zaidi ya urafiki tu, huku pia akimshukuru kwa kusimama upande wa faraja yake kila muda anapohitaji mtu wa kuzungumza na yeye.

Mchekeshaji huyo alisema kwamba kwa sasa hajui ni nini kitatoea huko mbeleni alipoulizwa iwapo anafaa kumpandisha hadhi Ruth K kutoka kuwa rafiki hadi kuwa mchumba, huku akisema kuwa hayuko tayari kabisa kuwa na mwanamke yeyote.

“Hakuna kitu poa kama kuwa na rafiki yaani bestee ni fiti kushinda kitu kingine chochote, ako kwangu kila muda kila siku. Lakini huwezi jua ya Mungu yamepangwa aje lakini kwa sasa mimi siko tayari kwa wanawake aina yoyote, sidai. Sasa hivi wacha float ipande,” Mulamwah alisema.

Akirejelea uhusiano wake na mama mtoto wake, Carrol Sonie ambao ulisambaratika miaka miwili iliyopita, Mulamwah alisema kuwa aliachwa bila kitu chochote kwa hiyo anahitaji muda Zaidi kujipanga kabla ya kujaribu kurejelea tena kwenye mduara wa mapenzi.

“Tuliachwa hatuna pesa wacha tufanye marekebisho kabla ya kurudi kwa huo uwanja. Bestee atulie afanye kazi, yeye amesainiwa chini ya Mulamwah Entertainment, naona anapiga kazi poa ako na endorsements, tunaendelea vizuri,” Mulamwah aliongeza.

Mulamwah hata hivyo hakuweza kufutilia mbali kabisa uwezekano wa kuchumbiana na mrembo Ruth K akisema;

“Yeye ni bestee kwa sasa, kwa hiyo kama vitu vingine vitakuwa pengine huko mbele mbele, huwezi jua,” alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved