logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kimani Ichung'wah: Handshake ya Ruto na Odinga iwe live kwa TV tumalize uhasama

Mapema wiki hii Ruto alisema yuko tayari kukutana na Odinga kufanya mazungumzo.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 July 2023 - 11:06

Muhtasari


• Mkereketwa huyo wa sera za serikali ya Kenya Kwanza alisema kwamba hatua hiyo itafanya kila Mkenya kujua ni nini viongozi hao watajadili.

Kimani Ichung'wah.

Mbunge wa Kikuyu ambaye pia ndiye kiongozi wa walio wengi katika bunge la kitaifa Kimani Ichung’wah ametoa sharti moja kwa rais Ruto pindi watakapokutana na kinara wa upinzani Raila Odinga ili kutafuta mwafaka wa taifa kutokana na maandamano.

Ichung’wah ambaye aliandamana na rais Ruto kule Kilifi katika ziara yake ya wiki moja kwenye mwambao wa Pwani alisema kwamba iwapo wawili hao watakutana, basi isiwe ni mkutano wa faragha bali uwe ni mkutano wa hadharani utakaofuatiliwa moja kwa moja na kila mtu.

Mkereketwa huyo wa sera za serikali ya Kenya Kwanza alisema kwamba hatua hiyo itafanya kila Mkenya kujua ni nini viongozi hao watajadili ili kupata hatima ya kuondoa taifa katika wimbi siasa za maandamano na kutoa nafasi ya uchumi kukua katika mazingira ya Amani.

Ichung’wah pia alisema kuwa hatua hiyo itahakikisha hakutakuwa na mazungumzo ya masuala ya kibinafsi bali ya kumjali kila Mkenya ambaye anaathirika kutokana na mwendelezo wa maandamano ambayo yamekuwa yakiitishwa na Azimio tangu mwezi Machi mwaka huu.

“Wananchi wa Magarini na Kenya mzima wamesema wanataka kuwa mashahidi wa yale mazungumzo ambayo mtakuwa nayo ili pasiwe na mambo ya kibinafsi. Yawe ni mazungumzo ya kufufua uchumi, mamabo yanayohusu wananchi wa kawaida wa Kenya,” alisema Ichung’wah.

Katika mkutano huo, Ruto aliwasuta vikali viongozi wa upinzani ambao walishiriki katika ibada ya kuwakumbuka waandamanaji waliofariki kutokana na maandamano hayo.

Ruto alisema kwamba viongozi wa upinzani wanastahili kuomba Kenya msamaha kwa kuandaa maandamano ambayo yalisababisha maafa, uharibifu wa mali ya umma na biashara za watu

Kiongozi wa taifa alisema kwamba machozi yao si ya kweli kwani kama si wao walioandaa na kufadhili maandamano hayo, basi mali na maisha ya watu hayangepotea.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved