logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Acha kumfuata Rais isivyofaa,'Wakili Donald Kipkorir kwa Gachagua

Ni wazi kuwa, tukio la mkutano wa kilele wa hali ya anga limemwaibisha pakubwa Gachagua.

image
na Radio Jambo

Habari04 September 2023 - 12:47

Muhtasari


  • Wakili huyo alisema kuwa ni wakati mwafaka wa kurejesha kamati ya mwongozo wa kitaifa na masuala ya kisiasa.
LIPA NA UKOME: Wakili Donald Kipokorir

Wakili Donald Kipkorir amemtaka naibu rais Rigathi Gachagua kujishughulisha na kuacha kumfuata rais katika kila shughuli hata pale ambapo hatakiwi kuongea.

Ni wazi kuwa, tukio la mkutano wa kilele wa hali ya anga limemwaibisha pakubwa Gachagua.

Naibu Rais Rigathi Gachagua alimfuata rais William Ruto kwenye kongamano la hali ya hewa KICC lakini kwa bahati mbaya hakupewa fursa ya kuzungumza.

Rais alitoa hotuba yake na kuelezea kujitolea kwake kwa masuala yanayohusu hatua za hali ya hewa.

Wakili huyo alisema kuwa ni wakati mwafaka wa kurejesha kamati ya mwongozo wa kitaifa na masuala ya kisiasa.

"Je, kuna jukumu la Naibu Rais wetu Rigathi Gachagua zaidi ya kumfuata Rais hata ikiwa Rais anaenda kuhesabu ng'ombe wake? Angalau tunajua DP wetu ni mtu anayeruka mapema na kukimbia mbio. Je, si wakati wa KAMATI YA MAZUNGUMZO kutoa jukumu halisi la utendaji kwa naibu rais? Tunaweza kurudisha Wizara ya Mwongozo wa Kitaifa na Masuala ya Kisiasa na kuifanya kuwa sehemu ya ofisi ya DP. (Wakenya waliozaliwa baada ya 1991 wanaweza wasijue tulikuwa na Wizara kama hiyo),"Kipkorir aliandika kwenye ukurasa wake rasmi wa Twitter.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved