logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kashfa ya kumpiga busu mchezaji yamfuta kazi kocha wa timu ya taifa ya wanawake ya Hispania

Katika taarifa yake, shirikisho la Hispania RFEF halijatoa sababu mahususi za kutimuliwa kwa Vilda.

image
na Radio Jambo

Habari06 September 2023 - 05:18

Muhtasari


•Ushindi wa Hispania ulifunikwa na kashfa ya rais wa shirikisho la soka nchini humo Rubiales kumbusu mshambuliaji Jenni Hermoso.

Jorge Vilda, kocha mkuu wa timu ya taifa ya wanawake iliyotwaa hivi majuzi Kombe la Dunia la Wanawake, amefukuzwa kazi kutokana na kashfa inayoendelea ya Luis Rubiales.

Ushindi wa Hispania ulifunikwa na kashfa ya rais wa shirikisho la soka nchini humo Rubiales kumbusu mshambuliaji Jenni Hermoso, jambo ambalo alisema lilikuwa la makubaliano.

Wengi katika benchi la ufundi la Vilda walijiuzulu huku wachezaji 81 wakikataa kuichezea Hispania baada ya tukio hilo. Rubiales amekataa kujiuzulu lakini amesimamishwa kwa muda na Fifa, shirikisho la soka duniani.

Katika taarifa yake, shirikisho la Hispania RFEF halijatoa sababu mahususi za kutimuliwa kwa Vilda.

Hata hivyo, RFEF imekuwa ikichunguza kama inaweza kumtimua Vilda - anayechukuliwa kuwa mshirika wa karibu wa Rubiales - tangu wiki iliyopita.

Alionekana akimpigia makofi Rubiales kwenye mkutano mkuu usio wa kawaida wa RFEF mapema mwezi Agosti - wakati Rubiales alipokuwa akisisitiza mara kwa mara kuwa hatajiuzulu na kusema angempa Vilda mkataba mpya..


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved