logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sifuna afichua kwa nini Passaris hakutimuliwa ODM

ODM ilisema azimio hilo lilifikiwa wakati wa Kamati Kuu ya Kitaifa ya chama hicho iliyofanyika Jumatano

image
na

Habari12 September 2023 - 12:10

Muhtasari


  • Siku ya Jumanne, Sifuna alisema kuwa Passaris alinyenyekea na kuomba msamaha alipofika mbele ya kamati ya nidhamu kuonesha sababu.
Mwakilishi wa kike Nairobi, Esther Passaris.

Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna amefichua sababu ya chama cha ODM kuchagua kumwepusha Mwakilishi wa kike wa Nairobi Esther Passaris shoka la kufurushwa ODM.

Siku ya Jumanne, Sifuna alisema kuwa Passaris alinyenyekea na kuomba msamaha alipofika mbele ya kamati ya nidhamu kuonyesha sababu.

"Passaris alikuja na kuomba radhi, hata hivyo, wabunge wengine walidharau wito kuhudhuria kikao cha nidhamu, mwingine alikuja na wakili wa UDA huku mwingine akishindwa kufika mbele ya kamati ya nidhamu," alisema.

Seneta huyo alibainisha kuwa wabunge hao wengine wa ODM walionyesha madharau ya wazi kwa chama hicho jambo ambalo lilichafua sura ya ODM na hivyo kutimuliwa.

Wiki iliyopita, chama cha ODM kilimtoza faini Passaris kwa kwenda kinyume na msimamo wa chama  kwa kupigia kura Mswada wa Fedha wa 2023, ambao sasa ni Sheria.

Chama hicho kilisema Passaris atalazimika kulipa Shilingi 250,000 kama faini kwa kukaidi chama kando na kuomba msamaha kwa maandishi ndani ya siku saba.

ODM ilisema azimio hilo lilifikiwa wakati wa Kamati Kuu ya Kitaifa ya chama hicho iliyofanyika Jumatano chini ya uongozi wa kiongozi wa Chama Raila Odinga.

"Kwamba Esther Passaris, Mbunge wa Kike katika Kaunti ya Nairobi akaripiwe kwa kukaidi moja kwa moja msimamo wa chama kuhusu Mswada wa Sheria ya Fedha wa 2023 na kwamba anapaswa kuomba radhi kwa maandishi ndani ya siku saba," chama hicho kilisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved