logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Majambazi wanaswa kwenye CCTV wakivamia Kanisa Embakasi

Wizi kanisani huku waalifu wakitoweka na sadaka ya kanisa

image
na

Habari13 September 2023 - 06:06

Muhtasari


•Polisi wameazisha uchunguzi  kuhusiana na wizi kwenye kanisa la Deliverance eneo la Embakasi.


Majambazi walionaswa kwenye kamera za CCTV wakivamia Kanisa moja eneo la Embakasi, wanasemekana kuiba bidhaa na pesa taslimu vyenye thamani ya shilingi milioni nne. 

Maafisa wa upelelezi jijini Nairobi wanachunguza kisa cha wizi katika Kanisa la Deliverance Embakasi kilichotokea alfajiri ya Jumatatu.

Kanda za CCTV zinaonyesha majambazi wanne wakiingia katika majengo ya kanisa na kutoroka na vifaa vya thamani. 

Picha zaonyesha kuwa majambazi wanne walifika eneo hilo mwendo wa saa saba na dakika 39 usiku wakiwa wamefuniko nyuso ili kuficha utambulisho wao. Waliswa na CCTV walimfunga mlinzi kabla ya kuingia kanisani.

Baadaye walionekana wakitoka na mabegi na vitu vingine vya thamani. Mmoja wa majambazi hao alinaswa akitafuta kitu katika eneo la juu la kanisa hilo na ndipo alipoona moja ya kamera za CCTV na kumulika mwanga wake.

Tukio hilo la wizi lilidumu kwa zaidi ya saa 2. Kulingana na wachungaji wa Kanisa la Deliverance, majambazi hao walichukua Ksh.400,000 kwenye sefu ya kanisa, ala za muziki, skrini tano, kibodi mbili, kichanganya sauti, kamera mbili, laptop mbili, kompyuta, na amplifaya mbili zinazokadiriwa kuwa za Ksh. milioni 4.

Wizi huo uliripotiwa katika Kituo cha Polisi cha Embakasi huku maafisa wa upelelezi wakianza uchunguzi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved