logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mkewe marehemu Mowzey Radio afukuzwa kwenye nyumba kisa deni la <em>rent</em> ya miezi 18

Mowzey Radio alifariki mwaka 2018.

image
na Radio Jambo

Habari27 September 2023 - 06:17

Muhtasari


• Hata hivyo, kutokana na sababu ambazo bado hazijajulikana, tangu Aprili 2022, Lilian Mbabazi hajatii suala la kulipa kodi yake.

• Hii ilimlazimu mwenye nyumba kuhusisha mamlaka, na mawakili wake walitoa notisi ya madai kwa Lilian Mbabazi.

Mjane wa Mowzey Radio, Lilian Mbabazi.

Mjane na mwimbaji marehemu Mowzey Radio kutoka nchini Uganda, Lilian Mbabazi yuko kwenye hatari ya kufukuzwa kutoka kwa ukodishaji wake kwa kushindwa kulipa malimbikizo yake ya kukodisha, vyombo vya habari nchini Uganda vimeripoti.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Bw. Sitran Deshpande, ambaye ni mwenye nyumba wa Lilian Mbabazi, mwimbaji huyo alikodisha nyumba hiyo tangu 21 Februari 2018 kwa kila mwezi Ugx 1.5M [Shilingi za Kenya elfu 59].

Hata hivyo, kutokana na sababu ambazo bado hazijajulikana, tangu Aprili 2022, Lilian Mbabazi hajatii suala la kulipa kodi yake.

Hii ilimlazimu mwenye nyumba kuhusisha mamlaka, na mawakili wake walitoa notisi ya madai kwa Lilian Mbabazi.

Wakili Sufian aliongeza kuwa licha ya kupata notisi hiyo ya madai, Lilian amekuwa akicheza kujificha akidai jinsi ambavyo amekuwa akipita na kurudi mjini hivyo kuwa vigumu kwake kutimiza ahadi zake.

Alibainisha zaidi kuwa pamoja na kwamba Lilian alidai kuwa bado ni mpangaji, aliacha mali zake zote kimya kimya; hata hivyo, mwimbaji huyo alikanusha hili wakati alipopigiwa simu na kushikilia kuwa alikuwa anatazamia kukutana na wahusika siku ya Alhamisi.

Lilian alizidi kudokeza kuwa amekuwa akitarajia pesa za kulipia kodi anayostahili kulipa, lakini jambo hilo limecheleweshwa.

Sufian alimtaka Lilian bila kukosa kujitokeza katika Kituo cha Polisi Konge siku ya Alhamisi, ili aweze kufungua nyumba kwa mamlaka kuchukua hatua.

Mowzey Radio, aliyejulikana kutoka kwa muziki wake na msanii mwenza Weasel, alifariki Februari mwaka 2018 baada ya mabishano na baunsa wa klabu moja jijini Kampala ambaye alisemekana kumdunda sakafuni na kufariki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved